16 Machi 2026 - 13:23
Source: ABNA
Habari zilizofichwa juu ya kuuawa na kujeruhiwa kwa askari 226 wa Marekani katika mashambulizi ya Iran

Vyombo vya habari vya Marekani, licha ya ukandamizaji mkubwa wa hasara na uharibifu wa askari wao katika vita na Iran, wamekiri kuuawa na kujeruhiwa kwa askari 226.

Kulingana na ripoti ya shirika la habari Abna, gazeti la Uingereza The Independent limeripoti kuwa katika mazingira ya sauti zinazosikika kutoka Marekani kuhusu kusitisha vita, inaonekana kuwa vita vya Trump na Iran vimepotea mwelekeo.
Gazeti la Wall Street Journal pia liliufichua hili kuwa hasara za kijeshi za Marekani zimeongezeka wiki mbili baada ya kuanza kwa mgogoro na Iran na katikati ya kuongezeka kwa mashambulizi ya pande zote katika eneo hilo.
Licha ya ukandamizaji mkubwa wa hasara na uharibifu wa Waamerika wakati wa vita, gazeti hili limeripoti kwa kumnukuu afisa wa Marekani kuwa askari 13 wa Marekani wameuawa tangu kuanza kwa vita, na wakati huo huo askari 213 wa Marekani wamejeruhiwa katika viwango tofauti.
Takwimu hizi zinatolewa huku vyanzo vya habari na wachambuzi katika eneo la usalama na jeshi wakikadir idadi halisi ya hasara ya jeshi la Marekani kuwa kubwa zaidi kuliko takwimu rasmi.
Kulingana na maafisa wa Marekani, idadi ya ndege za mafuta ya jeshi la anga la Marekani zilizoharibiwa au kuharibika imeongezeka hivi karibuni hadi angalau ndege 7. Ndege za mafuta za Marekani nchini Saudi Arabia zililengwa na mashambulizi ya makombora siku za hivi karibuni, jambo ambalo lilosababisha uharibifu wa baadhi ya ndege.
Maafisa wa Marekani walikiri kwa mtandao wa CBS News kuwa ndege zisizokuwa na rubani 11 za „MQ-Reaper“ zimeharibiwa tangu kuanza kwa vita hadi sasa.
Gazeti la The Cradle la Marekani pia liliiona uharibifu wa mifumo ya ulinzi wa anga, ikiwa ni pamoja na mifumo ya kupambana na makombora ya ballistic „THAAD“, ambayo kila kombo lake la kukinga gharama yake ni kati ya dola milioni 12 hadi 15, kuwa moja ya ishara muhimu zaidi ya hasara za kijeshi za Marekani katika vita hii.
Ripoti hiyo ilikiri kuwa pamoja na gharama za uendeshaji, mtandao wa radar ya Marekani katika Asia ya Magharibi, hasa UAE, Saudi Arabia na Jordan, umeathiriwa na mashambulizi ambayo yameathiri kwa kiasi kikubwa mfumo wa onyo la mapema wa Marekani na hasa Israeli.
Ripoti zinaonyesha kuwa Wizara ya Vita ya Marekani imemuarifu Bunge kuwa gharama ya wiki ya kwanza ya vita ilikuwa dola bilioni 11.3. Hii inatokea wakati Kituo cha Masomo ya Kimkakati na Kimataifa (CSIS) kinakadiria kuwa gharama hii imefika dola bilioni 16.5 siku ya kumi na mbili ya vita.

Your Comment

You are replying to: .
captcha