-
Chatham House: Makadirio ya Washington Kuhusu Vita Dhidi ya Iran Yalikuwa na Makosa
Taasisi ya utafiti ya Chatham House imesema kuwa baadhi ya dhana kuu za Washington kuhusu vita dhidi ya Iran hazikutimia, zikiwemo kuanguka kwa mfumo wa kisiasa wa Iran, kuilazimisha Tehran kujisalimisha kisiasa na kudhoofisha kwa kiwango kikubwa uwezo wake wa kimkakati.
-
Qalibaf: Waandishi wa Habari Ni Wapiganaji Wenye Maarifa Kama Ngome na Ukweli Kama Silaha
Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesema kuwa hatima ya mataifa haiamuliwi tu katika uwanja wa vita, bali pia katika uwanja wa simulizi, akisisitiza kuwa waandishi wa habari wana jukumu la kulinda ukweli, usalama wa kisaikolojia, utambulisho wa kitaifa na nguvu ya kiutamaduni ya taifa.
-
Wizara ya Ulinzi ya Iran: Iran Itaendelea Kuwa Imara na Yenye Nguvu Katika Uwanja wa Ulinzi
Wizara ya Ulinzi na Msaada kwa Vikosi vya Iran imesisitiza kuwa, katika mazingira ya vita mseto na operesheni za kisaikolojia za maadui, waandishi wa habari wana jukumu muhimu katika kusimulia ukweli kwa uaminifu, kulinda maoni ya umma na kuimarisha uwezo wa kitaifa wa kuzuia vitisho.
-
Yemen: Jeshi la Yemen Ladai Limewasambaratisha Maafisa wa Saudi Arabia na Makundi Yake ya Kijeshi
Chanzo cha ngazi ya juu nchini Yemen kimesema kuwa mashambulizi ya vikosi vya Yemen dhidi ya maeneo ya Al-Mokha na Ma’rib yamelenga mikusanyiko ya maafisa wa Saudi Arabia pamoja na maghala ya silaha, huku kikisisitiza kuwa harakati zote za kijeshi za Saudi Arabia zinaendelea kufuatiliwa kwa karibu.
-
Yemen: Maafisa wa Saudi Arabia Wauawa na Kujeruhiwa katika Mashambulizi ya Vikosi vya Yemen Mjini Al-Mokha
Vyanzo vya Al-Masirah vimeripoti kuwa maafisa kadhaa wa Saudi Arabia wameuawa na wengine kujeruhiwa katika operesheni ya hivi karibuni iliyolenga mikusanyiko ya vikosi vya Saudi Arabia katika eneo la Al-Mokha, huku milipuko na nguzo za moshi zikiendelea kuonekana katika maghala ya silaha yaliyoko katika pwani ya magharibi mwa Yemen.
-
Rosatom imeanza kurudisha wataalamu kwenye kiwanda cha nyuklia cha Bushehr
Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya serikali ya Rosatom alisema kwamba kampuni hiyo imeanza kurudisha wataalamu kwenye tovuti ya kiwanda cha nyuklia cha Bushehr nchini Iran.
-
Moscow: Waziri Mkuu wa Japan hakuwa na ujasiri wa kulitaja Marekani katika ushambuliaji wa atomiki
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Urusi alisema kwamba Sanae Takaichi hakuwa na ujasiri wa kusema ni nani aliyetupa bomu la atomiki kwenye nchi yake miaka 81 iliyopita.
-
Madai ya Wall Street Journal: Trump anataka kumaliza makabiliano na Iran
Gazeti la Wall Street Journal kwa kunukuu maafisa wa Marekani lilidai: Trump anataka kumaliza makabiliano na Iran na kutangaza ushindi dhidi ya nchi hii bila kufikia makubaliano ya nyuklia.
-
Upinzani wa Netanyahu dhidi ya mpango wa amani wa Gaza na kuundwa kwa nchi huru ya Palestina
Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni, akipinga mpango wa vifungu 15 uliowasilishwa na Baraza la Amani la Gaza, alidai: Maadamu mimi ni Waziri Mkuu, nchi ya Palestina haitaundwa.
-
Taarifa kali ya Shirika la Uhamasishaji wa Wananchi wa Iraq na kuunga mkono Faleh al-Fayyad
Shirika la Uhamasishaji wa Wananchi (Hashd al-Shaabi) wa Iraq limeuita shutuma zilizotolewa dhidi ya mwenyekiti wa shirika hili kuwa ni kashfa na kwa kusisitiza kwamba amri za tahadhari na kujiandaa zilitolewa kabla ya shambulio, limeripoti hatua za kisheria dhidi ya waenezaji uvumi.
-
Makubaliano ya Damascus na Moscow kuhusu mustakabali wa kambi mbili za Urusi
Wizara ya Mambo ya Nje ya utawala wa Julani ilitangaza kwamba Damascus na Moscow wamefikia maelewano ya makubaliano yanayobainisha mustakabali wa kambi mbili za Urusi.
-
Maafisa wa Saudi waliuawa na kujeruhiwa katika shambulio la Ansarullah dhidi ya «Mocha»
Baadhi ya vyanzo vimeripoti kuwa maafisa wa Saudi waliuawa na kujeruhiwa wakati wa shambulio la Ansarullah dhidi ya «Mocha».
-
Mpango wowote unaokiuka mamlaka ya Iran katika Mlango wa Hormuz hautakubaliwa
Makamu wa Spika wa Baraza la Mashauria la Kiislamu alisisitiza: Mpango au kauli yoyote inayokiuka mamlaka na usimamizi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Mlango wa Hormuz, haitakubalika kwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Amoli Larijani: Iran Haitaondoka kwenye Mlango wa Hormuz kwa Bei Yoyote
Mwenyekiti wa Baraza la Utambuzi wa Maslahi ya Mfumo alisisitiza: Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haitaondoka kwenye Mlango wa Hormuz kwa bei yoyote, na Mlango wa Hormuz hautarudi katika hali yake ya awali.
-
Amir Jahanshahi: Adui amepiga magoti mbele ya azimio la taifa la Iran
Kamanda wa Jeshi la Nchi Kavu alisema: Adui amepiga magoti mbele ya azimio la wanajeshi na taifa la Iran.
-
Wanafunzi wa Hawzat Zahra (sa) Washiriki katika Maombolezo ya Mtume Muhammad (saw) Jijini Dar es Salaam +Picha
Wanafunzi wa Hawzat Zahra (sa), chini ya usimamizi wa Jamiat Al-Mustafa (s) Tanzania, wameshiriki katika Majlisi ya maombolezo ya kumbukumbu ya kufariki dunia kwa Mtume Muhammad (saw), iliyofanyika katika Msikiti wa Ali Amir al-Mu’minin (as), eneo la Magomeni, Dar es Salaam.
-
Wanafunzi wa Hawzat Zahra (sa) Waadhimisha Arubaini ya Imam Hussein (as) kwa Kuonesha Mapenzi ya Vitendo kwa Ahlul-Bayt (as) +Picha
Baadhi ya wanafunzi mabinti wa Hawzat Zahra (sa) wamehudhuria katika nyumba ya mmoja wa wafuasi wa Ahlul-Bayt (as) na kuendesha Majlisi ya Arubaini ya Imam Hussein (as), wakisisitiza kuwa mapenzi ya kweli kwa Ahlul-Bayt (as) hayapaswi kubaki katika kauli na maneno pekee, bali yanapaswa kuonekana katika matendo, tabia na mwenendo wa maisha.
-
Msemaji wa IRGC: Tutaendelea kushikilia Mlango wa Hormuz hadi adui akubali masharti yetu yote
Brigedia Jenerali Mohbi amesema Iran itaendelea na mapambano hadi kufikia ushindi wa mwisho, akisisitiza kuwa waandishi wa habari walikuwa na nafasi muhimu katika kujenga uelewa wa ushindi, kuimarisha utamaduni wa upinzani na kudumisha umoja wa wananchi.
-
Araghchi: Iran itabaki thabiti kwenye ahadi ya mapambano; hatutasahau wala kusamehe uhalifu
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amesema Iran haitaruhusu damu za watu waliouawa kwa dhulma zisahaulike au kupuuzwa, akisisitiza kuwa nchi hiyo itaendelea kushikamana na njia ya mapambano na upinzani dhidi ya dhulma na mifumo ya kibabe, licha ya shinikizo zote.
-
Brigedia Jenerali Hassan Zadeh: Marekani na utawala wa Kizayuni wameshindwa kufikia malengo yao dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran
Kamanda wa Kikosi cha Muhammad Rasulullah (s) cha Tehran amesema kuwa kushindwa kwa Marekani na utawala wa Kizayuni kumedhihirisha uwezo mkubwa wa Iran, huku nguvu ya wananchi na utayari wa vikosi vya uhamasishaji ukiifanya Iran kuwa miongoni mwa nguvu kuu katika eneo na duniani.