Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Zawadi ya Hijja ni miongoni mwa matukio ya kipekee yaliyoambatana na Kongamano la 30 la Jamiat Al-Mustafa (s), lililofanyika tarehe 20 Mei, 2025. Katika kongamano hili, wahudumu wa Qur’an Tukufu kutoka nyanja mbalimbali walituzwa zawadi nono, ikiwa ni ishara ya kutambua mchango wao katika kuieneza na kuitumikia Qur’an.
22 Mei 2025 - 14:02
News ID: 1691566
Miongoni mwa zawadi hizo, zawadi ya safari ya ibada ya Hijja ilijitokeza kuwa ya kipekee na yenye mvuto mkubwa. Sheikh Abdul Majid Nasir ndiye aliyebahatika kuibuka mshindi wa zawadi hii adhimu, akipata baraka na utukufu wa Qur’an Tukufu kupitia ushindi wake huu wa kipekee.
Your Comment