Kwa Mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul Bayt (a.s) -ABNA- Sherehe ya kufikia umri wa kubalehe na kutekeleza Hukumu za Kisheria (Taklif) kwa kundi la Wasichana imefanyika katika Mji Mkuu wa Senegal, Dakar, kwa juhudi za Jumuiya ya Wanawake ya Bibi Fatimah Zahra (s.a) chini ya Baraza la Wanazuoni wa Ahlul-Bayt nchini Senegal.
Ayatollah Reza Ramezani, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul Bayt (a.s), ambaye yuko nchini Senegal kwa mwaliko wa viongozi wa kidini wa nchi hiyo, alikuwa mgeni maalum katika hafla hiyo.
Sherehe hii ilikuwa ya heshima kubwa kwa wasichana waliofikia umri wa balehe, na ilijumuisha hotuba, mawaidha ya kidini, burudani ya kimaadili, na kuwapa zawadi wasichana waliofikia umri wa taklif (umri wa kuwajibika kidini kwa kuchunga na kutekeleza hukumu na sheria za kidini).
Your Comment