Kambi hii iliambatana na maonesho ya Taasisi mbalimbali zilizotambulisha huduma na mafanikio yao, zikiwemo Taasisi ya Kimataifa ya Al-Mustafa (sa) na Mashirika mengine ya maendeleo na kidini.

3 Agosti 2025 - 22:15

Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Huduma maalum za uchunguzi na matibabu ya macho zilitolewa (kuanzia tarehe: 01/08/2025 - 03/08/2025) kwa Wananchi chini ya uangalizi wa Madaktari Bingwa wa Macho, kwa uratibu wa Jumuiya ya Khoja Shia Ithnaashari ya Dar es Salaam, kwa kushirikiana na wataalamu wa afya kutoka ndani na nje ya nchi.

Kambi ya Macho na Maonesho ya Taasisi za Kidini na Kijamii Yaleta Mshikamano na Huduma kwa Jamii Dar es Salaam

Kambi hii iliambatana na maonesho ya Taasisi mbalimbali zilizotambulisha huduma na mafanikio yao, zikiwemo Taasisi ya Kimataifa ya Al-Mustafa (sa) na Mashirika mengine ya maendeleo na kidini.

Wageni kutoka Taasisi za Kishia na zisizo za Kishia hapa nchini walihudhuria pia, na kuonesha mshikamano wao katika utoaji wa huduma za kijamii.

Tukio hili limekuwa jukwaa mwafaka la kuimarisha ushirikiano katika sekta ya afya, elimu, na mahusiano kati ya Taasisi za Kidini na Kijamii.

Kambi ya Macho na Maonesho ya Taasisi za Kidini na Kijamii Yaleta Mshikamano na Huduma kwa Jamii Dar es Salaam

Your Comment

You are replying to: .
captcha