Viongozi wa JMAT walisisitiza kwamba maridhiano na mshikamano ni msingi wa maendeleo ya taifa, huku wakihimiza jamii kuendeleza mazungumzo ya upendo, heshima na mshikamano.
Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT) imeandaa kongamano maalumu la Maridhiano na Amani lililofanyika katika Kata ya Vijibweni, Wilaya ya Kigamboni, Mkoa wa Dar-es-Salaam.
Kongamano hili lilijumuisha viongozi wa dini, wazee wa jamii, vijana pamoja na wadau mbalimbali wa amani, ambapo mijadala na mada ziliwasilishwa kuhusu:
- Umuhimu wa mshikamano na Ushirikiano wa kijamii,
- Kudumisha amani na maelewano katika jamii,
- Kukuza ushirikiano baina ya makundi tofauti ya kijamii na kidini,
- Kuelimisha vijana juu ya kuepuka vitendo vya vurugu na misimamo mikali.
Viongozi wa JMAT walisisitiza kwamba maridhiano na mshikamano ni msingi wa maendeleo ya taifa, huku wakihimiza jamii kuendeleza mazungumzo ya upendo, heshima na mshikamano.
Aidha, washiriki walipata nafasi ya kuuliza maswali, kutoa maoni na kushiriki mijadala ya wazi juu ya namna bora ya kuimarisha uhusiano wa kijamii na kudumisha amani katika familia na jamii kwa ujumla.
Your Comment