"Upandishaji wa Bendera hii unatufunza kuwa Mtume Muhammad (s.a.w.w) ametufundisha Amani, Upendo na Kushikamana. Kuishi kwa misingi hiyo kutaiwezesha nchi yetu kuwa ya amani, yenye mshikamano na mapenzi ya kweli kati ya wananchi wake"

6 Septemba 2025 - 01:00

Bendera ya Mtume Muhammad (s.a.w.w) Yapandishwa Masjid Ghadiir Kigogo – Ujumbe wa Amani na Umoja Watolewa +Picha

Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Dar es Salaam – Katika kuadhimisha Maulidi ya Mtume Muhammad (s.a.w.w), tukio la heshima la kupandisha Bendera ya Mtume Muhammad (s.a.w.w) limefanyika leo katika Msikiti wa Ghadiir, uliopo Kigogo Post, jijini Dar es Salaam.

Bendera ya Mtume Muhammad (s.a.w.w) Yapandishwa Masjid Ghadiir Kigogo – Ujumbe wa Amani na Umoja Watolewa +Picha

Akizungumza wakati wa shughuli hiyo, Sheikh Jalala alieleza kuwa:

"Upandishaji wa Bendera hii unatufunza kuwa Mtume Muhammad (s.a.w.w) ametufundisha Amani, Upendo na Kushikamana. Kuishi kwa misingi hiyo kutaiwezesha nchi yetu kuwa ya amani, yenye mshikamano na mapenzi ya kweli kati ya wananchi wake".

Shughuli hiyo imelenga kuwahamasisha waumini na jamii kwa ujumla kuenzi mafunzo ya Mtume (s.a.w.w) kwa vitendo, hasa katika kipindi hiki muhimu cha Wiki ya Umoja wa Kiislamu.

Maulidi rasmi ya Mtume Muhammad (s.a.w.w) yatafanyika siku ya Jumatano, tarehe 10 Septemba 2025, ambapo waumini na wananchi wote wanakaribishwa kushiriki katika hafla hiyo adhimu ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Rehma kwa walimwengu wote.

Bendera ya Mtume Muhammad (s.a.w.w) Yapandishwa Masjid Ghadiir Kigogo – Ujumbe wa Amani na Umoja Watolewa +Picha

Your Comment

You are replying to: .
captcha