Mohammad Baqer Qalibaf, Mwenyekiti wa Bunge la Shura la Kiislamu (Majlisi), katika ziara yake mjini Qom, alikutana na Maraji‘ wakuu wa Taqlid wakiwemo Ayatollah Makarem Shirazi, Ayatollah Javadi Amoli, Ayatollah Shobeiri Zanjani, na Ayatollah Subhani.
Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Mohammad Baqer Qalibaf, Mwenyekiti wa Bunge la Iran (Majlisi ya Shura ya Kiislamu), katika ziara yake ya hivi karibuni mjini Qom, alikutana na kuzungumza na Marajii wakuu wa Taqlid ambap ni pamoja na: Ayatollah al-Uzma Shobeiri Zanjani, Ayatollah Abdullah Javadi Amoli, Ayatollah Naser Makarem Shirazi, na Ayatollah Jafar Subhani, ambao ni miongoni mwa Marajii wa juu kabisa wa Taqlid (Maraji‘ al-Taqleed Al-Idham - مراجع التقليد العظام).
Katika mikutano hii, mada zilizojadiliwa ni pamoja na masuala ya uchumi, maisha ya kila siku, na ripoti ya utendaji wa Bunge la Shura ya Kiislamu.
Aidha, Mwenyekiti Qalibaf alitembelea Haram Tukufu ya Bi Fatimah Masuma (s.a) na kuhudhuria sherehe ya kuenzi walimu na wasimamizi wa taasisi ya utafiti wa Kiislamu ya Bunge.
Kwa picha zaidi za mkutano huu, unaweza kutembelea ripoti za picha zilizochapishwa na vyombo mbalimbali vya habari vya Iran, kama ABNA na Tasnim News Agency.
Your Comment