Kadhia ya Fadak na Haki za Imam Ali (AS): Katika hotuba yake, alibainisha kuhusu Kadhia ya Fadak, ardhi aliyopewa na Mtume Muhammad (SAW) ambayo baadaye ilichukuliwa kwa dhulma. Pia alifafanua jinsi Bibi Fatimah (SA) alivyoshiriki kikamilifu na kwa ujasiri katika kupinga unyang'anyi huo na kupinga waporaji wa ukhalifa wa Imam Ali (AS), akasimama kidete kulinda haki kwa ajili ya kuzipata Radhi za Allah (SWT).

15 Novemba 2025 - 17:42

Majlis Kuhusu Historia na Fadhila za Bibi Fatimah (SA) | Chuo cha Kidini cha Mabinti wa Kiislamu cha Hazrat Zainab (sa) – Kigamboni, Dar-es-s +Picha

Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Dar-es-salaam, Tanzania – Katika muktadha wa maombolezo ya shahada ya Sayyidat Fatimah (SA), Chuo cha Kidini cha Mabinti wa Kiislamu cha Hazrat Zainab (SA) kilifanya somo maalumu kuhusiana na fadhila na maisha ya Bibi Fatimah Al-Zahra (SA).

Khatibu wa Majlisi

Kikao kiliongozwa na Samahat Sayyid Wajih, ambaye alisisitiza umuhimu wa maisha na tabia njema za Bibi Fatimah (SA) katika nyanja mbalimbali: maadili, kiroho, na kijamii. Alieleza jinsi Bibi Fatimah (SA) alivyotumia maisha yake kikamilifu katika njia ya haki inayoridhia Allah (SWT), na kushirikiana na mumewe Imam Ali (AS) katika kusaidia jamii na kushughulikia changamoto za kila siku.

Majlis Kuhusu Historia na Fadhila za Bibi Fatimah (SA) | Chuo cha Kidini cha Mabinti wa Kiislamu cha Hazrat Zainab (sa) – Kigamboni, Dar-es-s +Picha

Historia na Matukio Muhimu

Khatibu alikumbusha matukio yaliyojiri baada ya kifo cha Mtume Muhammad (SAWW), akibainisha masaibu makubwa yaliyompata Binti huyu kipenzi wa Mtume. Aidha, alizungumzia tofauti zilizopo kuhusu tarehe ya kifo chake na sababu za tofauti hizo.

Fadhila na Mfano wa Kuigwa

Samahat Sayyid Wajih alisisitiza fadhila za Bibi Fatimah (SA), akibainisha kuwa yeye ni mfano wa kuigwa kwa kila Muislamu, mwanamke na mwanaume, na kwamba alikuwa dalili ya haki na hoja kwa wafuasi wa Ahlul-Bayt (AS).

Kadhia ya Fadak na Haki za Imam Ali (AS)

Katika hotuba yake, alibainisha kuhusu Kadhia ya Fadak, ardhi aliyopewa na Mtume Muhammad (SAWW) ambayo baadaye ilichukuliwa kwa dhulma. Pia alifafanua jinsi Bibi Fatimah (SA) alivyoshiriki kikamilifu na kwa ujasiri katika kupinga unyang'anyi huo na kupinga waporaji wa ukhalifa wa Imam Ali (AS), akasimama kidete kulinda haki kwa ajili ya kuzipata Radhi za Allah (SWT).

Majlis Kuhusu Historia na Fadhila za Bibi Fatimah (SA) | Chuo cha Kidini cha Mabinti wa Kiislamu cha Hazrat Zainab (sa) – Kigamboni, Dar-es-s +Picha

Ujumbe Muhimu kwa Wanawake

Majlisi hii ilitolewa kama somo muhimu kwa wanawake, ikisisitiza jinsi wanawake wanaweza kujifunza kutoka kwa maisha na ujasiri wa Bibi Fatimah (SA) katika kudumisha haki, maadili, na imani thabiti.

Kwa ujumla 

Kikao kilimalizika kwa wito wa kuendelea kuthamini sala ya jamaa, kujifunza maadili, na kuiga tabia nzuri za Bibi Fatimah (SA) katika maisha ya kila siku. Wanafunzi walionekana kuhamasika na kupata motisha ya kiroho na maadili kutokana na somo hili.

Your Comment

You are replying to: .
captcha