Kwa taufiki ya Mwenyezi Mungu (s.w.t), mitihani yote imeendeshwa kwa utaratibu uliopangwa na kukamilika kwa mafanikio. Uongozi wa madrasa mbalimbali umeonyesha ushirikiano mkubwa, huku walimu na wasimamizi wakifanya kazi kwa uadilifu na bidii kuhakikisha kwamba kila hatua ya zoezi hili inafanikishwa kwa ufanisi.

18 Novemba 2025 - 23:24

Ripoti ya Mitihani ya Mwisho wa Mwaka 2025 - Hujjatul Asr Society of Tanzania +Picha

Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt(as) -ABNA- Taasisi ya Hujjatul Asr Society of Tanzania, chini ya usimamizi wa Maulana Sayyid Arifu Naqvi Mwenyezi Mungu amuhifadhi, imefanikisha kwa mafanikio makubwa zoezi la mitihani ya mwisho wa mwaka 2025 kwa madrasa zote zilizo chini ya taasisi katika maeneo mbalimbali ya Tanzania.

Ripoti ya Mitihani ya Mwisho wa Mwaka 2025 - Hujjatul Asr Society of Tanzania +Picha

Lengo la Mitihani
Mitihani hii imelenga kukusanya takwimu na kutathmini kiwango cha uelewa wa wanafunzi na waumini kuhusu elimu ya Uislamu, ikizingatia mafundisho sahihi ya Ahlul Bayt (a.s). Zoezi hili limekuwa chachu ya kuboresha mitaala, mbinu za ufundishaji, na kuongeza ubora wa elimu katika madrasa zote zinazoratibiwa na taasisi.

Ripoti ya Mitihani ya Mwisho wa Mwaka 2025 - Hujjatul Asr Society of Tanzania +Picha

Utekelezaji wa Zoezi
Kwa taufiki ya Mwenyezi Mungu (s.w.t), mitihani yote imeendeshwa kwa utaratibu uliopangwa na kukamilika kwa mafanikio. Uongozi wa madrasa mbalimbali umeonyesha ushirikiano mkubwa, huku walimu na wasimamizi wakifanya kazi kwa uadilifu na bidii kuhakikisha kwamba kila hatua ya zoezi hili inafanikishwa kwa ufanisi.

Ripoti ya Mitihani ya Mwisho wa Mwaka 2025 - Hujjatul Asr Society of Tanzania +Picha

Shukurani na Dua
Taasisi inamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kukamilisha jukumu hili muhimu. Shukurani za dhati pia zinatolewa kwa watumishi wote wa Hujjatul Asr Society kwa kujitolea kwao katika kufikisha ujumbe wa Ahlul Bayt (a.s). Aidha, tunawashukuru wale wote wanaotoa juhudi zao za hali na mali kwa ajili ya kuendeleza harakati za tabligh chini ya mwavuli wa taasisi.

Ripoti ya Mitihani ya Mwisho wa Mwaka 2025 - Hujjatul Asr Society of Tanzania +Picha

Tunaomba Mwenyezi Mungu awazidishie taufiki, afya na uwezo katika kuendelea kulitumikia Dini Tukufu ya Uislamu.

Ripoti ya Mitihani ya Mwisho wa Mwaka 2025 - Hujjatul Asr Society of Tanzania +Picha

Your Comment

You are replying to: .
captcha