Mapambo hayo yamewekwa katika uga wa haram, njia za waumini, na maeneo ya ibada kama ishara ya: 1_Furaha ya Kiislamu, 2_Upendo kwa Ahlul-Bayt (a.s), 3_Na heshima kubwa kwa binti wa Mtume Muhammad (s.a.w.w).

8 Desemba 2025 - 00:00

Picha: Haram Tukufu ya Maimamu Wawili Jawadain (a.s) Yapambwa kwa Maua Kwa Furaha ya Kusubiri Kuzaliwa kwa Bibi Fatima Zahra (s.a)

Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (a.s) -ABNA- Baghdad - Iraq | Haram takatifu ya Maimamu wawili watukufu, Imam Muhammad Al-Jawad (a.s) na Imam Ali Al-Hadi (a.s), iliyopo katika mji wa Kadhimiyah, Baghdad – Iraq, imepambwa kwa maua maridadi na mapambo ya furaha kwa ajili ya kuukaribisha msimu mtukufu wa maadhimisho ya kuzaliwa kwa Mwanamke bora zaidi kuliko Wanawake wote wa Ulimwengu mzima, Sayyidat Fatima Zahra (a.s), Binti Kipenzi wa Mtume Muhammad (saww).

Mapambo hayo yamewekwa katika uga wa haram, njia za waumini, na maeneo ya ibada kama ishara ya:

1_Furaha ya Kiislamu

2_Upendo kwa Ahlul-Bayt (a.s)

3_Na heshima kubwa kwa binti wa Mtume Muhammad (s.a.w.w).

Waumini wengi wameendelea kufika kwa wingi kutoa:

1_Ziyara

2_Dua

3_Na kushiriki katika shamrashamra za kiroho kuelekea kumbukumbu ya tukio hilo tukufu.

Sherehe hizi huambatana pia na:

1_Majlisi za mawaidha

2_Qasida na tenzi za mapenzi kwa Bibi Zahra (a.s)

3_Na matendo ya hisani kwa wahitaji.

Picha: Haram Tukufu ya Maimamu Wawili Jawadain (a.s) Yapambwa kwa Maua Kwa Furaha ya Kusubiri Kuzaliwa kwa Bibi Fatima Zahra (s.a)

Your Comment

You are replying to: .
captcha