Tukio hili ni hatua nyingine katika kuimarisha daraja la maelewano, ushirikiano na kuheshimiana baina ya mataifa mawili rafiki, likiwa pia kumbusho la wajibu wa kimataifa wa kusimama upande wa amani, maadili, na ustawi wa jamii.

11 Desemba 2025 - 23:58

Rais Dr.Samia Suluhu Hassan Ampokea Balozi Mteule wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Ikulu Chamwino - Dodoma | Ni Hatua Mpya ya Ushirikiano wa Kimaendeleo

Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Balozi Mteule wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Tanzania, Mohammad Javad Hemmatpanah, ameweka historia mpya katika safari yake ya kidiplomasia baada ya kuwasili Ikulu Chamwino, Mkoani Dodoma, kwa ajili ya kuwasilisha Hati zake za Utambulisho kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, tarehe 11 Desemba 2025.

Rais Dr.Samia Suluhu Hassan Ampokea Balozi Mteule wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Ikulu Chamwino - Dodoma | Ni Hatua Mpya ya Ushirikiano wa Kimaendeleo

Mara baada ya kuwasili Ikulu, Balozi Hemmatpanah alipokelewa kwa heshima za kitaifa na kusaini Kitabu Maalum cha Wageni, ukiwa ni ishara ya kuanza rasmi muhula wake wa uwakilishi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran hapa nchini.

Katika tukio hilo lenye umuhimu mkubwa wa kimataifa na kidiplomasia, pande zote mbili zimetumaini kuimarika zaidi kwa uhusiano wa kihistoria uliopo kati ya Tanzania na Iran, hususan katika maeneo ya elimu, afya, uchumi, nishati, utamaduni, na masuala ya kiulimwengu yanayohusu amani na haki za watu.

Rais Dr.Samia Suluhu Hassan Ampokea Balozi Mteule wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Ikulu Chamwino - Dodoma | Ni Hatua Mpya ya Ushirikiano wa Kimaendeleo

Tukio hili ni hatua nyingine katika kuimarisha daraja la maelewano, ushirikiano na kuheshimiana baina ya mataifa mawili rafiki, likiwa pia kumbusho la wajibu wa kimataifa wa kusimama upande wa amani, maadili, na ustawi wa jamii.

Rais Dr.Samia Suluhu Hassan Ampokea Balozi Mteule wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Ikulu Chamwino - Dodoma | Ni Hatua Mpya ya Ushirikiano wa Kimaendeleo

Mwisho kabisa, viongozi hao wanatarajiwa kuendeleza mazungumzo ya kina kuhusu ajenda mbalimbali za ushirikiano zinazolenga kuwanufaisha wananchi wa pande zote mbili.

Rais Dr.Samia Suluhu Hassan Ampokea Balozi Mteule wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Ikulu Chamwino - Dodoma | Ni Hatua Mpya ya Ushirikiano wa Kimaendeleo

Your Comment

You are replying to: .
captcha