Timu ya taifa ya Iran imeelekea Mexico kwa maandalizi ya mwisho ya Kombe la Dunia 2026, ikitarajia kuanza kampeni yake kwa mechi dhidi ya New Zealand baada ya kuweka kambi katika mji wa Tijuana.
Kwa Mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) - ABNA -, timu ya taifa ya mpira wa miguu ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imeondoka kuelekea nchini Mexico kwa ajili ya kuendelea na maandalizi ya kushiriki katika mashindano ya Kombe la Dunia 2026. Timu hiyo imeondoka baada ya kukamilisha kambi ya mazoezi nchini Uturuki na inatarajiwa kuweka makazi yake katika mji wa Tijuana, Mexico, kabla ya kuanza mechi zake za hatua ya makundi.
Kwa mujibu wa taarifa zilizochapishwa na vyombo mbalimbali vya habari, Iran iliamua kuhamishia kambi yake ya Kombe la Dunia nchini Mexico kutokana na changamoto za masuala ya viza kwa baadhi ya maafisa wa ujumbe wake, huku wachezaji na benchi la ufundi wakitarajiwa kushiriki kikamilifu katika mashindano hayo.
Timu ya Iran, chini ya kocha Amir Ghalenoei, inatarajiwa kuanza kampeni yake ya Kombe la Dunia kwa mechi dhidi ya New Zealand kabla ya kukutana na Belgium na Egypt katika hatua ya makundi.
Your Comment