Wanafunzi 144 wa Jamiatul Mustafa, wakiongozana na msimamizi wao, walishiriki majlisi ya maombolezo ya Muharram katika Msikiti wa Amirul Muuminin (AS) uliopo Mgomeni, Dar es Salaam. Majlisi hiyo ilijumuisha muhadhara wa Sheikh Hujjatul Islam wal-Muslimin Aydarus, kisomo cha Qur'ani Tukufu na maombolezo ya Imam Hussein (AS), ikiwa ni sehemu ya kuhuisha ujumbe wa Karbala wa haki, uadilifu na kujitolea katika njia ya Mwenyezi Mungu.