Amesema kuwa uongo mwingi kuhusu Iran unatolewa na taasisi zinazopingwa na msimamo wa Iran wa kusimama dhidi ya Marekani na Israel. Hata hivyo, baada ya vita vya siku kumi na mbili, wanafikra wengi duniani wamekiri wazi kwamba Iran ndilo taifa pekee lililosimama dhidi ya dhulma kwa njia ya kivitendo, si kwa maneno tu.
Msafara wa Kimataifa wa Ustahimilivu (al-Sumud) umetangaza kuwa Jeshi la Majini la utawala wa Kizayuni limeushambulia Msafara wa Uhuru uliokuwa ukielekea Gaza kwa lengo la kuvunja mzingiro unaoendelea dhidi ya eneo hilo.