Majini
-
Jeshi la Iran latangaza hatua ya 13 ya Operesheni "Saa'iqah"; lasema limelenga meli ya Marekani kwa kombora la cruise
Jeshi la Iran limetangaza kuwa katika hatua ya 13 ya Operesheni "Saa'iqah", vikosi vyake vya majini vilirusha kombora la cruise kuelekea meli ya kijeshi ya Marekani kaskazini mwa Bahari ya Hindi, likisema hatua hiyo ilisababisha meli hiyo kujiondoa kutoka eneo hilo.
-
kamanda wa jeshi la majini la Iran: muqawama haujafungwa tena na mipaka ya kijiografia
Kamanda wa Jeshi la Majini la Iran, Admiral Shahram Irani, amesema kuwa Muqawama sasa umevuka mipaka ya kijiografia, akisisitiza kuwa mataifa na vikosi vya Muqawama vinaendelea kuimarisha umoja na mshikamano katika kukabiliana na changamoto.
-
Iran Yalaani Vitisho vya Marekani dhidi ya Oman, Yasema Usalama wa Hormuz Unalindwa kwa Mujibu wa Sheria za Kimataifa
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amelaani kauli za vitisho za Marekani dhidi ya Oman akisisitiza kuwa ushirikiano wa Iran na Oman katika kulinda usalama wa usafiri wa majini katika Mlango wa Hormuz unafuata sheria za kimataifa na unalenga kulinda maslahi ya jamii ya kimataifa.
-
Kamanda wa Jeshi la Majini la Iran Akutana na Wenzake wa Urusi na Saudi Arabia Kando ya Mazoezi ya Majini ya Milan 2026 nchini India
Kamanda wa Jeshi la Majini la Iran, Admiral Shahram Irani, alikutana kando ya mazoezi ya Milan 2026 nchini India na viongozi wa Jeshi la Majini la Urusi na Saudi Arabia, ambapo walijadili ushirikiano wa kijeshi, usalama wa baharini, na kuimarisha uhusiano wa kimkakati kati ya nchi hizo.
-
Profesa wa Chuo Kikuu cha Indonesia katika mahojiano na ABNA:
“Iran ni mfano wa kipekee wa maendeleo ya kisayansi na uimara dhidi ya vikwazo – ni lazima mtu aione kwa macho yake”
Amesema kuwa uongo mwingi kuhusu Iran unatolewa na taasisi zinazopingwa na msimamo wa Iran wa kusimama dhidi ya Marekani na Israel. Hata hivyo, baada ya vita vya siku kumi na mbili, wanafikra wengi duniani wamekiri wazi kwamba Iran ndilo taifa pekee lililosimama dhidi ya dhulma kwa njia ya kivitendo, si kwa maneno tu.
-
Jeshi la Majini la Israel lavamia Msafara wa Uhuru uliokuwa ukielekea Gaza
Msafara wa Kimataifa wa Ustahimilivu (al-Sumud) umetangaza kuwa Jeshi la Majini la utawala wa Kizayuni limeushambulia Msafara wa Uhuru uliokuwa ukielekea Gaza kwa lengo la kuvunja mzingiro unaoendelea dhidi ya eneo hilo.