Kufunguliwa kwa milango ya Bwawa la Atatürk nchini Uturuki kumesababisha mafuriko makubwa katika maeneo ya Deir ez-Zor na Raqqa nchini Syria, huku zaidi ya hekta 24,000 za mashamba zikiharibiwa na maelfu ya wananchi kulazimika kuhama makazi yao.
Maelfu ya wananchi mjini Mexico City waliungana katika maandamano makubwa yaliyopewa jina “Mexico kwa Palestina”, wakilaani jinai za utawala wa Kizayuni na uungaji mkono wa Marekani, huku wakidai kusitishwa kwa mauaji ya kimbari Gaza na kutumwa haraka kwa misaada ya kibinadamu.