Lebanon inakabiliwa na uvamizi hatari wa Kizayuni: Akirejea mashambulizi ya mara kwa mara ya Israel kusini mwa Lebanon, alisema: “Lebanon inakabiliwa na uvamizi wa hatari na wa kupanua mipaka wa utawala wa Kizayuni. Lazima tukabiliane nao kwa kila njia na mbinu. Adui huyu haheshimu makubaliano yoyote.”
Beirut – Baadhi ya wanasiasa na wabunge wa Lebanon wamewasilisha malalamiko rasmi dhidi ya Sheikh Naeem Qassem, Katibu Mkuu wa Hizbullah, baada ya hotuba yake ya hivi karibuni aliyoituhumu serikali ya Lebanon kwa kutaka kuisalimisha nchi mikononi mwa Israel.