Oman
-
Mazungumzo ya ngazi ya pili yasiyo ya moja kwa moja kati ya Iran na Marekani imeendelea Siku ya Jumanne huko Geneva, Uswisi
Raundi ya pili ya mazungumzo ya nyuklia kati ya Iran na Marekani imefanyika Siku ya Jumanne katika Ubalozi wa Oman uliopo mjini Geneva, Uswisi. Mazungumzo haya yanafanyika katika hali ambayo bado kuna ukosefu wa imani, unaotokana na kile kinachoelezwa kuwa ni misimamo na tabia zinazokinzana kutoka upande wa Washington—hali ambayo inaendelea kuwa moja ya changamoto kuu katika mchakato huu wa mazungumzo.
-
Reuters: Iran Yasisitiza Haki ya Kurutubisha Uranium Katika Mazungumzo ya Muscat
Reuters yaripoti kuwa Iran imesisitiza haki yake ya kurutubisha uranium katika mazungumzo ya Muscat, huku ikionyesha utayari wa kujadiliana kuhusu kiwango cha urutubishaji au kuanzishwa kwa consortium ya kikanda, na ikaongeza kuwa masuala ya makombora hayakujumuishwa kwenye ajenda ya mazungumzo.
-
Araqchi: Mazungumzo kati ya Iran na Marekani yatafanyika Ijumaa mjini Muscat
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ametangaza kuwa mazungumzo ya nyuklia kati ya Iran na Marekani yatafanyika katika mji mkuu wa Oman, Muscat.
-
Zaher Al-Mahrouqi katika mahojiano na ABNA:
Mfano wa Somaliland utaenea kwa nchi nyingine / Taa ya kijani kwa hatua hii italigharimu eneo kwa gharama kubwa za kiusalama!
Mwandishi na mchambuzi wa masuala ya kisiasa kutoka Oman, katika mahojiano na ABNA, ameielezea hatua ya Israel ya kuitambua Somaliland kuwa ni jaribio hatari la kulazimisha uhalisia mpya dhidi ya wananchi wa Palestina. Alisisitiza kuwa uamuzi huu si tu ukiukaji wa wazi wa haki za Wapalestina, bali pia unaweza kutathminiwa kuwa sehemu ya mradi wa kuliondoa Gaza wakazi wake na kufanya uhandisi wa idadi ya watu katika eneo.
-
Mufti wa Oman:
“Inasikitisha kuwa waandishi wa habari wanauawa Gaza na baadhi wanaendelea kuwaunga mkono wavamizi”
Mufti wa Oman amelaani mauaji ya waandishi wa habari katika mji wa Gaza yaliyofanywa na jeshi la Israel, na kutamka masikitiko yake juu ya kuendelea kwa baadhi ya watu na nchi kuunga mkono wavamizi.
-
Ziara ya Pezeshkian nchini Oman | Mizinga 21 yafyatuliwa kwa heshima ya Rais wa Iran mjini Muscat
Dkt. Massoud Pezeshkian, Rais wa Iran, amefanya ziara nchini Oman kwa madhumuni ya kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi, kisiasa na kitamaduni. Alipowasili katika uwanja wa ndege wa Muscat, alipokelewa na maafisa wa ngazi za juu wa nchi hiyo. Sherehe rasmi ya mapokezi ilifanyika katika Kasri ya Al-Alam kwa uwepo wa Sultan wa Oman, ambapo mizinga 21 ilifyatuliwa kwa heshima ya Rais wa Iran.
-
Raundi mpya ya mazungumzo kati ya Iran na Marekani itafanyika Ijumaa hii Mjini Rome, Italia
Raundi ya tano ya mazungumzo kati ya Iran na Marekani inatarajiwa kufanyika siku ya Ijumaa mjini Rome, Italia. Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ametangaza kuwa nchi yake imekubali pendekezo la Oman kwa ajili ya kikao hiki. Aidha, alisisitiza kuwa ujumbe wa Iran katika mazungumzo haya umejikita katika kulinda haki za taifa hilo na kuhakikisha kuondolewa kwa vikwazo vilivyowekwa dhidi ya Iran.