Balozi wa zamani wa kitamaduni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Lebanon na mshauri wa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt (a.s) alisema: “Ikiwa Imam Musa Sadr alikuwa mwanzilishi wa taasisi za kijamii na kitamaduni za Waislamu wa Kishia nchini Lebanon, basi Sayyid Isa Tabatabaei ndiye aliyepuliza roho ya mapambano ndani ya jamii ya Kishia na kuifanya roho hiyo kuwa sehemu ya utambulisho wao. Kutokana na jitihada zake, ndipo mapambano ya kisasa ya Lebanon yalipozaliwa - mapambano ambayo baadaye yalifikia kilele chake katika kuunga mkono dhana na malengo ya Palestina.”