Unabii

  • Ni vipi Fatima Zahra (a.s) Alikuwa Mpenzi na Mpendwa Zaidi Katika Maisha ya Ali (a.s)?

    Ni vipi Fatima Zahra (a.s) Alikuwa Mpenzi na Mpendwa Zaidi Katika Maisha ya Ali (a.s)?

    Katika baadhi ya nyakati, mtu humtambulisha nafsi yake kwa kutaja nasaba yake na watu wakubwa. Hivyo ndivyo alivyofanya Amirul-Mu'minin Ali (a.s) katika mojawapo ya khutba zake baada ya kurejea kutoka vita vya Nahrawan. Ali (a.s) alisema: “Mimi ni mume wa Bibi Batul, Bibi wa wanawake wa ulimwengu, Fatima aliye mchamungu, msafi, mtukufu, mwongofu, mpendwa wa Mpenzi wa Allah, bora wa mabinti wake na mchanga wa roho ya Mtume wa Allah (s.a.w.).” Kutaja kwa Imam Ali (a.s) daraja la juu la Bibi Zahra (a.s) baada ya kujinasabisha na mwanamke huyu mtukufu ni kusisitiza nafasi kuu ya bibi huyu mbele ya mtu mkubwa kama Ali (a.s).

  • Ufafanuzi wa Kina na Maridhawa Juu ya Suala la Unabii Baina ya Waislamu na Wakristo

    Ufafanuzi wa Kina na Maridhawa Juu ya Suala la Unabii Baina ya Waislamu na Wakristo

    Sheikh Dk.Alhad Mussa Salum: "Wakristo wanaposema, au tunaposikia ikisemwa, au anapoitwa mtu kuwa ni Nabii au Nabii Mkuu, anaitwa hivyo kwa Istilahi ipi?! Hili ndio swali la msingi kujiuliza?. Anaitwa hivyo kwa Istilahi yetu sisi Waislamu au kwa istilahi yao hao ndugu zetu Wakristo?!. Kwa sababu katika suala la UNABII kila watu wana Istilahi zao".