Mazungumzo ya nyuklia kati ya Marekani na Iran yamekamilika bila mafanikio ya msingi, huku Iran ikikataa kusitisha urutubishaji wa uranium au kuhamisha vifaa vyake nje ya nchi. Tehran imesisitiza kuwa utajirishaji ndani ya Iran ni mstari mwekundu, wakati Washington ikisisitiza haitakubali Iran kubaki na uwezo wowote wa silaha za nyuklia. Kwa hali hii, duru ijayo ya mazungumzo itaamua hatima ya diplomasia kati ya pande hizo mbili.
Kiongozi wa Mapinduzi alipozungumzia mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja na Wamarekani, alisisitiza kuwa: Kauli ya Wamarekani kwamba 'hawataruhusu Iran irutubishe urani' ni upuuzi mtupu. Hakuna mtu yeyote nchini anayesubiri ruhusa ya huyu au yule. Jamhuri ya Kiislamu itaendelea kufuata sera na njia yake kama kawaida.