Abu Ubaidah, msemaji wa Brigedi za Al-Qassam, ametoa wito kwa vijana wa Palestina kuongeza operesheni za mapambano dhidi ya Israel katika Ukingo wa Magharibi, huku akipongeza uthabiti wa wananchi wanaokabiliana na mashambulizi ya walowezi wa Kizayuni.
Wizara ya Awqaf (Wakfu) na Mambo ya Kidini imesema kuwa walowezi walivamia Msikiti wa Hajjah Hamidah uliopo Salfit, kaskazini mwa Ukingo wa Magharibi, na kulitaja tukio hilo kuwa “jinai ya kinyama na shambulio la wazi dhidi ya hisia za Waislamu.”