Main Title
29 Aprili 2024
Wanafunzi wanaunga mkono Palestina waendelea kukamatwa Marekani
Katika siku za hivi karibuni, polisi nchini Marekani wamewatia mbaroni wanafunzi wa vyuo vikuu wasiopungua 900 wanaoiunga mkono Palestina na wanaopinga mauaji ya kimbari ya utawala ghasibu na haramu wa Israel katika Ukanda wa Gaza
29 Aprili 2024
Raisi: Mkono wa chuma hauwezi kuzima harakati ya wanachuo Magharibi ya kuunga mkono Palestina
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, harakati ya wanafunzi, maprofesa na wasomi wa nchi za Magharibi za kuwaunga mkono wananchi wanaodhulumiwa wa Palestina ni tukio kubwa lenye muelekeo mipana ambalo haliwezi kuzimwa kwa ukandamizaji, vipigo, kamatakamata na vitendo vya utumiaji mabavu.
29 Aprili 2024
Kuongezeka mauzo ya nje ya bidhaa zisizokuwa za mafuta za Iran
Maonesho ya 6 ya uwezo wa kuuza nje bidhaa za Jamhuri ya Kiislamu ya Iran yalianza Jumamosi hapa mjini Tehran kwa hotuba ya Rais Ebrahim Raisi.
29 Aprili 2024
Iran leo inaadhimisha Siku ya Taifa ya Ghuba ya Uajemi
Wananchi wa Iran leo wanaadhimisha Siku ya Kitaifa ya Ghuba ya Uajemi, ambayo ni nembo ya misimamo isiyoyumba ya kukabiliana na njama za baadhi ya nchi za kikanda za kutaka kubadilisha jina la eneo hilo la kistratijia la maji.
29 Aprili 2024
Kamanda wa IRGC: Iran mdhamini wa usalama wa Ghuba ya Uajemi
Kamanda wa Kikosi cha Wanamaji cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amesema mkakati wa Iran ni kuendeleza amani, usalama na udugu katika Ghuba ya Uajemi na Mlango Bahari wa Hormuz.
29 Aprili 2024
Rais wa Syria: Mshikamano wa nchi za Kiarabu unapelekea kupatikana utulivu katika eneo
Rais wa Syria amesema kuwa kuwepo mshikamamo baina ya nchi za Kiarabu na kutekeleza hatua za pamoja kutapelekea kupatikana amani na uthabiti katika eneo.
29 Aprili 2024
UNRWA: Takriban watoto 17,000 wametenganishwa na familia zao Gaza kufuatia vita vya Israeli
Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA) limebainisha wasiwasi wake juu ya hali inayozidi kuzorota ya watoto wa Kipalestina katika Ukanda wa Gaza, huku Israel ikiendeleza vita vyake vya mauaji ya kimbari dhidi ya eneo hilo linalozingirwa.
29 Aprili 2024
Wanajeshi 14 wa Israel waangamizwa, wajeruhiwa katika operesheni ya muqawama Gaza
Takriban wanajeshi watatu wa utawala katili wa Israel wameangamizwa na wengine 11 kujruhiwa vibaya katika eneo la vita kati kati mwa Ukanda wa Gaza, huku vikosi vya muqawama au mapambano ya Kiisalmu Palestina vikiendelea kulisababishia hasara kubwa jeshi katili la utawala huo.
28 Aprili 2024
Mkuu wa UNRWA atahadharisha: Israel inajiandaa kufanya shambulio kubwa la kijeshi Rafah
Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Kipalestina UNRWA amesema, utawala wa Kizayuni unajiandaa kwa operesheni kubwa ya kijeshi katika mji wa Rafah ulioko kusini mwa Ukanda wa Ghaza.
28 Aprili 2024
Mjukuu wa Mandela: Afrika Kusini imepata msukumo kutokana na uthabiti wa Wapalestina
Mjukuu wa Nelson Mandela amesema Afrika Kusini imetiwa moyo na kupata msukumo kutokana na istikama na uthabiti wa Wapalestina; na kwa sababu hiyo ikaileta hoja ya piganio lao mbele ya Jamii ya Kimataifa.
28 Aprili 2024
Ukandamizaji hautawanyamazisha waandamanaji wanaoiunga mkono Palestina nchini Marekani
Uwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika ofisi ya Umoja wa Mataifa mjini Geneva umelaani vikali ukandamizaji unaoendelea dhidi ya waandamanaji wanaoiunga mkono Palestina katika vyuo vikuu vya Marekani, na kusisitiza kwamba ghasia dhidi ya waandamanaji wa amani hazitawanyamazisha.
28 Aprili 2024
Kan'ani: Iran ni katika washirika muhimu wa amani duniani
Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamuu ya Iran amesema, Iran imegeuza vikwazo kuwa fursa ya kuimarisha na kuendeleza uwezo wake wa kiulinzi na kijeshi, na ni miongoni mwa washirika muhimu wa jami ya kimataifa katika kuhakikisha amani na usalama wa kieneo na kimataifa na kupambana na ugaidi wa kimataifa.
28 Aprili 2024
Makamu wa Rais wa Iran asisitiza kuendeleza uhusiano na nchi za Afrika
Makamu wa kwanza wa rais wa Iran amesema kuwa, kustawisha uhusiano na nchi za Kiafrika imekuwa stratijia ya Iran tangu ulipopatikana ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu mwaka 1979.
28 Aprili 2024
Kushadidi mgogoro wa kisiasa katika baraza la mawaziri la utawala wa Kizayuni
Kuendelea maandamano ya mitaani huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu (Israel), tofauti za kimtazamo kati ya wapinzani na baraza la mawaziri na kuongezeka uwezekano wa Mahakama ya Kimataifa ya Uadilifu kutoa amri ya kumkamata Benjamin Netanyahu kumezidisha mzozo wa kisiasa huko Tel Aviv.
28 Aprili 2024
Kan'ani: Sauti ya kuvurugika mifupa ya Uzayuni duniani inasikika zaidi hivi sasa
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema, sauti ya kuvurugika mifupa ya Uzayuni duniani inasikika zaidi sasa hivi kuliko wakati mwingine wowote.
28 Aprili 2024
UN yaunga mkono maandamano ya wanafunzi wa vyuo vikuu Marekani ya kuwatetea watu wa Gaza
Stephen Dujaric Msemaji wa Umoja wa Mataifa jana Ijumaa alisema katika radiamali yake kwa maandamano yanayoendelea kufanywa na wanafunzi wa vyuo vikuu huko Marekani katika kuwaunga mkono watu wa Gaza na kupinga mauaji ya kimbari dhidi ya wakazi wa eneo hilo kwamba: Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ni mfuasi na mungaji mkono mkubwa wa uhuru wa kujieleza, ikiwa ni pamoja na huko Marekani; na anaunga mkono haki ya wananchi ya kufanya maandamano kwa amani.
28 Aprili 2024
Amnesty International: Ubaguzi wa apartheid wa Israel dhidi ya Wapalestina hauwezi kukanushwa
Katibu Mkuu wa Shirika la Msamaha Duniani la Amnesty International amesema kuwa, utawala wa Israel umetekeleza ubaguzi wa apartheid dhidi ya Wapalestina. Agnes Callamard amesema kuwa, ameshangazwa mno na utumiaji mabavu wa kimfumo wa utawala ghasibu wa Israel.
28 Aprili 2024
Wapalestina 37 wauawa shahidi katika mashambulio ya Israel huko Gaza
Wapalestina 37 wameuawa shahidi katika mashambulio ya anga ya utawala wa Kizayuni wa Israel katikati na kusini mwa Ukanda wa Gaza.
28 Aprili 2024
Uwezekano wa ICC kutoa waranti wa kukamatwa Netanyahu kwa mauaji ya Ghaza umeitia tafrani Israel
Baraza la mawaziri la utawala haramu wa Kizayuni wa Israel limeingiwa na tafrani na wasi wasi mkubwa juu ya uwezekano wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) kutoa waranti wa kukamatwa waziri mkuu wa utawala huo Benjamin Netanyahu na maafisa wengine waandamizi kwa kuhusika na jinai za vita vya miezi kadhaa vya mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Ghaza uliozingirwa.
28 Aprili 2024
Viongozi wa makundi ya Palestina wakutana Istanbul, Uturuki kujadili yanayojiri Ghaza
Viongozi wa Harakati za Hamas, Jihadul-Islami na Vuguvugu la Wananchi la Ukombozi wa Palestina wamekutana kujadili yanayojiri kwenye medani za mapambano na za kisiasa za Palestina na vita katika Ukanda wa Ghaza.