Main Title
2 Mei 2024
Jitihada za China za kuleta maridhiano ya kitaifa Palestina
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China ametangaza kuwa kufuatia mkutano wa wawakilishi wa harakati za Palestina za Hamas na Fat'h mjini Beijing, pande mbili zimefikia makubaliano ya kujadili maridhiano ya kitaifa huko Palestina.
2 Mei 2024
Utawala wa Kizayuni umewatia nguvuni mamia ya wafanyakazi wa Kipalestina
Vyanzo vya habari vya Palestina vimeripoti kuwa Wazayuni maghasibu wamewatia mbaroni zaidi ya wafanyakazi elfu tano wa Kipalestina katika mwaka huu wa 2024 huku hali za kiafya za raia hao wa Kipalestina zikitajwa kuwa mbaya.
2 Mei 2024
Colombia yaamua kuvunja uhusiano na Israel kwa sababu ya mauaji ya kimbari ya Ghaza
Colombia imeamua kuvunja uhusiano wake wa kidiplomasia na utawala wa Kizayuni wa Israel kutokana na vita vya kinyama na mauaji ya kimbari yanayoendelea kufanywa na utawala huo haramu dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Ghaza.
2 Mei 2024
Baada ya uamuzi wa kihistoria wa Colombia; Hamas yataka mataifa yote kuvunja uhusiano na Israel
Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imepongeza na kukaribisha kwa mikono miwili uamuzi wa Colombia wa kuvunja uhusiano wake na utawala haramu wa Israe.
30 Aprili 2024
UN: Kombora la balestiki la Korea Kaskazini limetumika kushambulia mji wa Kharkiv, Ukraine
Wachunguzi wa vikwazo wa Umoja wa Mataifa wameiambia kamati ya vikwazo ya Baraza la Usalama la umoja huo kuwa, mabaki ya kombora yaliyopatikana katika mji wa Kharkiv nchini Ukraine mnamo Januari 2 yanatokana na kombora la balestiki la Korea Kaskazini aina ya Hwasong-11.
30 Aprili 2024
Wanachuo wanaoitetea Palestina Marekani watiwa nguvuni Texas, wasimamishwa masomo Columbia
Polisi nchini Marekani wamekabiliana na wanafunzi wa chuo kikuu katika mji wa Austin jimboni Texas, na kuwakamata makumi ya watu baada ya kubomoa mahema yaliyowekwa kupinga na kulalamikia vita vya kinyama na mauaji ya kimbari yanayofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina wa Ghaza.
30 Aprili 2024
Mwanasiasa mkongwe wa Uingereza: Sheria ya Rwanda inaharibu sifa ya Uingereza
Alfred Dubs mwanasiasa mkonge ambaye ni mjumbe katika Bunge la Malodi la Uingereza amesema kuwa mpango wa kuhamishia nchini Rwanda kutoka Uingereza raia wanaotafuta hifadhi si sahihi na hautafanikiwa.
30 Aprili 2024
IRGC: Usaidizi wa nchi 10 duniani kwa Wazayuni haukufua dafu mbele ya Shambulio la Iran
Msemaji wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amesema nchi 10 ziliusaidia utawala wa Kizayuni katika ulinzi wa anga ili kukabiliana na operesheni ya Ahadi ya Kweli ya kuutia adabu utawala huo, lakini hatimaye Iran ya Kiislamu iliisambaratisha na kuishinda mifumo hiyo ya ulinzi ya nchi hizo zinazotajika.
30 Aprili 2024
Iran na nchi za Afrika zaunda kamati ya ushirikiano katika sekta ya kilimo
Wizara ya Jihadi ya Kilimo ya Iran imetangaza kuwa Jamhuri ya Kiislamu na nchi za Afrika zimekubaliana kuunda kamati ya ushirikiano wa pamoja katika sekta ya kilimo.
30 Aprili 2024
Ghuba ya Uajemi ni nyumba yetu
Jumatatu ya jana tarehe 10 Ordibehesht, 1403 Hijria, sawa na Aprili 29, 2024 ilisadifiana na kumbukumbu ya kutimuliwa wakoloni wa Kireno katika maji ya kusini mwa Iran mwaka 1622 Miladia.
30 Aprili 2024
Ujumbe wa Algeria na azma yake ya kustawisha ushirikiano wa kiteknolojia na Iran
Mkuu wa Chama cha Wafanyabiashara wa Algeria amepongeza maendeleo ya kiteknolojia ya Iran na kusisitiza azma ya nchi hiyo ya kuendeleza ushirikiano wa kiteknolojia na Iran.
30 Aprili 2024
Kuharibiwa Gaza; Jinai za utawala wa Kizayuni dhidi ya kizazi cha sasa na kijacho
Mwezi wa saba wa vita unamalizika tangu utawala wa Kizayuni uanzishe vita na mauaji ya kimbari dhidi ya Ukanda wa Gaza, huku mashambulizi ya kila siku ya utawala huo yakisababisha maafa na uharibifu mkubwa wa miundombinu ya mji na afya katika ukanda huo.
30 Aprili 2024
Wapalestina zaidi ya 8,500 wametiwa nguvuni Ukingo wa Magharibi tangu Oktoba 7 hadi sasa
Jumuiya ya kushughulikia mateka wa Kipalestina imetangaza katika ripoti yake kwamba utawala ghasibu wa Kizayuni wa Israel umewatia nguvuni Wapalestina 8,505 katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan tangu tarehe 7 Oktoba 2023 mara baada ya kutekelezwa operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa.
30 Aprili 2024
Balozi zote za Israel zawekwa kwenye hali ya tahadhari kuhofia waranti wa ICC wa jinai za vita vya Ghaza
Wizara ya Mambo ya Nje ya utawala wa Kizayuni wa Israel imeziagiza balozi zake duniani kote kuwa tayari kwa madhara yanayoweza kutokea iwapo Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) itatoa waranti wa kukamatwa maafisa wa utawala huo kwa uhalifu wa kivita na ukiukaji wa haki za binadamu dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Ghaza.
30 Aprili 2024
Vituo vya utafiti vya Ulaya vyaiunga mkono Palestina na kuiwekea vikwazo Israel
Vituo vya utafiti barani Ulaya vimeuwekea vikwazo utawala wa Kizayuni na kuunga mkono malengo ya Palestina. Viituo hivyo vya utafiti vya Ulaya pia vimelaani jinai za utawala huo unaotekeleza mauaji ya kimbari dhidi ya watu wa Gaza.
30 Aprili 2024
Ujumbe wa Hamas umeondoka Cairo kwa ajili ya mashauriano zaidi
Ujumbe wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) umeondoka Cairo, mji mkuu wa Misri ili kufanya mashauriano zaidi kuhusu pendekezo jipya lililotolewa kwa ajili ya kubadilishana mateka.
29 Aprili 2024
Intelijinsia Marekani: Putin hakuamuru kuuliwa Navalny
Jarida la Wall Street limezinukuu duru za kiintelijinsia za Marekani na kuripoti kuwa Rais Vladmir Putin wa Russia hakuagiza kuuawa mwanasiasa wa upinzani wa nchi hiyo, Alexei Navalny, aliyefia gerezani mwezi Februari mwaka huu.
29 Aprili 2024
Abbas: Utawala wa Kizayuni umeangamiza asilimia 75 ya Ukanda wa Gaza
Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina amesema kuwa utawala wa Kizayuni wa Israel umeangamiza asilimia 75 ya nyumba, miundombinu ya barabara, vyuo vikuu, misikiti na miundo msingi mingine ya Ukanda wa Gaza.
29 Aprili 2024
Wasiwasi wa Russia kuhusu kusambaa zaidi ugaidi kutokea Afghanistan
Waziri wa Ulinzi wa Russia ametangaza kuwa tishio kuu kwa Asia ya Kati ni kutoka kwa makundi ya kigaidi yenye misimamo mikali yenye makao makuu nchini Afghanistan.
29 Aprili 2024
Mgombea wa uchaguzi wa rais Marekani atiwa nguvuni katika maandamano ya watetezi wa Palestina
Polisi nchini Marekani imemtia nguvuni mgombea wa kiti cha urais katika uchaguzi wa mwaka huu nchini humo ambaye alikuwa katika maandamano ya kuiunga mkono Palestina yaliyofanyika katika Chuo Kikuu cha Washington.