Main Title
6 Mei 2024
Seneta wa Marekani: Wanafunzi wanaopinga vita vya Ghaza wamesimama upande sahihi wa historia
Bernie Sanders, Seneta wa kujitegemea anayewakilisha jimbo la Vermont nchini Marekani amewasifu wanafunzi wa vyuo vikuu vya nchi hiyo wanaopinga vita katika Ukanda wa Ghaza na kusema, wanafunzi hao wamesimama upande sahihi wa historia.
6 Mei 2024
Borrell: Marekani imepoteza nafasi yake katika Nidhamu ya Dunia ya pande kadhaa
Mkuu wa Sera za Nje wa Umoja wa Ulaya Josep Borrell amesema, Marekani imepoteza nafasi yake katika Nidhamu ya Dunia ya pande kadhaa.
6 Mei 2024
Polisi waondoa kambi ya waungaji mkono wa Palestina katika Chuo Kikuu cha California Kusini
Polisi wa Los Angeles huko Marekani wameondoa kambi ya watu wanaoiunga mkono Palestina pambizoni mwa uwanja wa chuo kikuu cha California kusini.
6 Mei 2024
Russia yatangaza, imeharibu kambi 2 za magaidi nchini Syria
Wizara ya Ulinzi ya Russia imetangaza kuwa imeharibu kambi mbili za magaidi wanaosaidiwa na Marekani huko magharibi mwa Syria.
6 Mei 2024
Askofu Mkuu wa Azerbaijan, Iran alaani kuvunjiwa heshima Qurani Sweden
Askofu Mkuu wa Kanisa la Armenia katika eneo la Azerbaijan la kaskazini magharibi mwa Iran ameashiria kitendo cha karibuni cha kuchoma moto nakala ya Qur'ani tukufu nchini Sweden na kulaani vitendo hivyo vya kuyavunjia heshima matukufu ya kidini.
6 Mei 2024
Iran yatathmini njia za kuimarisha uhusiano wake na Tunisia
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu inachunguza njia na majukwaa ya kuimarisha zaidi uhusiano wa pande mbili kati yake na Tunisia.
6 Mei 2024
Rais wa Iran: Matukio ya Gaza yamefichua sura halisi ya Magharibi
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, matukio ya Gaza yamefichua sura halisi ya Wamagharibi na kuonyesha mgongano uliopo kati ya kambi ya watu sharifu, na tabaka la wanafunzi wenye uelewa wa vyuo vikuu na mrengo wa uovu wa viongozi wakorofi na wanaokanyaga sheria, haki na uhuru wa binadamu wa nchi za Magharibi.
6 Mei 2024
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu: Hija ya mwaka huu ni Hija ya kujitenga na adui Mzayuni na waungaji mkono wake
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema, kwa kuzingatia Aya za Qur'ani Tukufu na kumbukumbu ya jina lililobarikiwa la Nabii Ibrahim (AS), ibada ya Hija ya mwaka huu inapaswa kuwa zaidi ya Hija ya kila mwaka, na inabidi iwe Hija na kutangaza kujitenga na adui wa Waislamu, Mzayuni mtenda uhalifu na wafuasi wake.
6 Mei 2024
Vyombo vya habari Iraq vimekatazwa kutumia jina 'Israel', vinauita 'Utawala wa Kizayuni'
Vyombo vya habari vya Iraq vimeacha kutumia neno "Israel" kumaanisha utawala wa Tel Aviv na badala yake vinatumia msamiati "Utawala wa Kizayuni" katika hatua ya kuonyesha mshikamano na Wapalestina kwa miezi kadhaa sasa.
6 Mei 2024
Kiongozi wa HAMAS: Makubaliano ya usitishaji vita lazima yakomeshe uchokozi wa utawala wa Israel
Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amesisitiza kuwa, harakati hiyo inataka kufikia makubaliano kamili na jumuishi ili kukomesha uchokozi wa utawala ghasibu wa Kizayuni.
6 Mei 2024
Kuanza awamu ya nne ya operesheni ya jeshi la Yemen dhidi ya meli zinazokwenda Israel
Sambamba na maandamano ya wananchi wa Yemen katika miji tofauti ya nchi hiyo ya kuwaunga mkono watu wa Gaza, msemaji wa jeshi la Yemen ametangaza habari ya kuanza awamu ya nne ya operesheni za nchi hiyo kwa ajili ya kuwatetea wananchi wa Palestina na kusisitiza kuwa: Wigo wa mashambulizi ya Yemen yutapanuka kuanzia Bahari ya Mediterania hadi sehemu yoyote ambayo nchi hii inaweza kuzifikia meli zinazoelekea Palestina inayokaliwa kwa mabavu (Israel).
6 Mei 2024
Askari 3 wa Israel waangamizwa katika shambulio la HAMAS
Wanajeshi watatu wa utawala wa Kizayuni wa Israel wameangamizwa katika shambulizi la ulipizaji kisasi lililofanywa na Mujahidina wa Brigedi za Izzuddin al-Qassam, tawi la kijeshi la Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS.
5 Mei 2024
Meli ya kivita ya Iran yaelekea ncha ya kusini ya sayari ya dunia
Meli ya kivita ya iliyoundwa ndani ya nchi na wataalamu Wairani inayomilikiwa na Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (IRGC) imevuka mstari wa latitudo nyuzi sifuri, Ikweta, na kuelekea katika ncha ya kusini ya sayari ya dunia.
5 Mei 2024
Abdollahian: Utawala wa Kizayuni wa Israel kamwe hauwezi kuwa halali kwa kupita zama
Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, Utawala wa Israel si serikali halali na utawala huo wa kibaguzi unaoukalia kwa mabavu Palestina kamwe hauwezi kuwa halali kwa kupita zama.
5 Mei 2024
Irani, Misri zinajadili kukuza uhusiano, kukomesha ukatili wa Israel
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na Misri wamejadili njia zinazowezekana za kustawisha uhusiano wa pande mbili na kukomesha jinai zinazofanywa na Israel dhidi ya watu wa Palestina hususan katika Ukanda wa Gaza.
5 Mei 2024
Safari ya Abdollahian Gambia kushiriki mkutano wa OIC wa kujadili changamoto za Waislamu hasa Palestina
Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran yupo Banjul, mji mkuu wa Gambia kwa ajili ya kushiriki katika mkutano wa 15 wa Wakuu wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu, OIC.
5 Mei 2024
Iran yapongeza uamuzi wa Uturuki kukata uhusiano wa kibiashara na utawala wa Israel
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amepongeza uamuzi wa serikali ya Uturuki wa kukata uhusiano wa kiuchumi na kibiashara na utawala wa Kizayuni wa Israel unaotekeleza mauaji ya kimbari dhidi ya watu wa Ukanda wa Gaza.
5 Mei 2024
Mottaki: Operesheni dhidi ya Israeli ilifichua 'sehemu ndogo ya uwezo wa Iran'
Waziri wa zamani wa Mambo ya Nje wa Iran Manouchehr Mottaki anasema operesheni ya kulipiza kisasi ya Iran dhidi ya Israel ilionyesha "sehemu ndogo" tu ya uwezo wa Iran wa kukabiliana na utawala huo ghasibu.
5 Mei 2024
Ufaransa yamzuia daktari Muingereza aliyekuwa Gaza kuingia nchini humo kutoa ushahidi
Daktari mpasuaji mwenye uraia pacha wa Uingereza na Palestina, Ghassan Abu Sittah ambaye ni shahidi wa uhalifu wa kivita wa Israel katika Ukanda wa Gaza, amezuiwa kuingia Ufaransa, ambako alipangwa kuhutubia Baraza la Seneti kuhusu hali ya Gaza.
5 Mei 2024
Maandamano yanaendelea kote duniani kulaani hujuma ya Israel dhidi ya Gaza
Miji ya nchi mbalimbali duniani jana Jumamosi ilishuhudia maandamano ya kulaani uvamizi na vita vya Israel dhidi ya watu wa Ukanda wa Gaza huko Palestina, ambapo washiriki wametoa wito wa kusitishwa mapigano haraka iwezekanavyo.