Main Title
11 Mei 2024
Abdollahian: Iran iko tayari kushirikiana na Ulaya kwa kuzingatia maslahi ya pamoja
Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, Tehran iko tayari kushirikiana na Ulaya kwa kuzingatia maslahi ya pande mbili.
11 Mei 2024
Askari wa Israel waendelea kuangamizwa na wanamuqawama Gaza
Wanajeshi wengine watano wa utawala wa Kizayuni wa Israel wameangamizwa katika shambulizi la ulipizaji kisasi lililofanywa na Mujahidina wa Brigedi za Izzuddin al-Qassam, tawi la kijeshi la Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS katika Ukanda wa Gaza.
11 Mei 2024
Borrell: Nchi 4 za Ulaya kulitambua taifa la Palestina
Mkuu wa Sera za Nje wa Umoja wa Ulaya amethibitisha kuwa nchi nne za Ulaya zitaitambua Palestina kama taifa huru.
11 Mei 2024
Watu 200 wafariki dunia kwa janga la mafuriko nchini Afghanistan
Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa, kwa akali watu 200 wamefariki duniani kwa mafuriko kaskazini mwa Afghanistan.
10 Mei 2024
Iran yakosoa vitisho na mashinikizo wawakilishi wa Kongresi dhidi ya mahakama ya ICC
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa ni fedheha na jambo lenye kutia wasiwasi kuona baadhi ya wawakilishi wa Kongresi na Seneti ya Marekani wanatoa vitisho na kuwashinikiza waendesha mashtaka na majaji wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC).
10 Mei 2024
Iran: Lugha ya Kifarsi kufundishwa katika Vyuo Vikuu vya Zimbabwe
Waziri wa Sayansi, Utafiti na Teknolojia wa Iran ametangaza utayarifu wa Jamhuri ya Kiislamu wa kuanza kufunza lugha ya Kifarsi katika Vyuo Vikuu vya Zimbabwe.
10 Mei 2024
Kiongozi Muadhamu: Kushiriki uchaguzi ni wajibu wa kitaifa wa kila mmoja
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kushiriki katika uchaguzi ni wajibu wa kitaifa kwa wananchi wote.
10 Mei 2024
Rais wa Iran: Makombora na uwezo wa kijeshi wa Iran haviwezi kujadiliwa
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametoa mkono wa baraka kwa mnasaba wa kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa wajukuu wa Mtume wetu Muhammad (saw), Bibi Fatima Masoumah na kaka yake, Imam Ridha (as) na kusema: Kama ilivyosisitizwa na Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, uwezo wa kijeshi na vielelezo vya mamlaka ya mfumo wa Kiislamu hapa nchini haviwezi kujadiliwa au kufanyiwa biashara kwa njia yoyote ile.
10 Mei 2024
Kaburi jingine la umati lafukuliwa huko Gaza, "miili isiyo na vichwa yapatikana"
Wahudumu wa afya kaskazini mwa Gaza wametoaa miili mingine katika kaburi jingine la umati katika Hospitali ya Shifa. Hii ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na ofisi ya vyombo vya habari huko Ukanda wa Gaza. taarifa hiyo imeongeza kuwa miili hiyo iliyotolewa katika kaburi la umati imekutwa bila ya vichwa.
10 Mei 2024
Yemen yashambulia meli 3 za Waisraeli katika Ghuba ya Aden, Bahari ya Hindi
Msemaji wa Jeshi la Yemen amesema vikosi vya jeshi la majini, anga na makombora vya nchi hiyo vimezishambulia meli tatu zenye uhusiano na Israel kama sehemu ya kampeni ya baharini ya kuwaunga mkono na kuwatetea Wapalestina katika Ukanda wa Gaza.
10 Mei 2024
Muqawama wa Iraq washambulia maeneo ya kistratajia ya Israel, Eilat
Harakati ya Kiislamu ya Iraq imetangaza kuwa imeshambulia maeneo ya kistratajia ya Israel katika mji wa Eilat, ulioko kusini mwa Palestina inayokaliwa kwa mabavu.
10 Mei 2024
Al Houthi: Yemen italenga meli zenye uhusiano na Israel bila kujali zinakoenda
Kiongozi wa harakati ya Ansarullah ya Yemen, Abdul Malik al-Houthi, amesema vikosi vya jeshi la nchi hiyo vitalenga meli za kampuni yoyote inayohusiana na kusambaza au kusafirisha bidhaa hadi Israel bila kujali zinakoelekea.
10 Mei 2024
Iran: Tutaangalia upya sera ya nyuklia iwapo uwepo wetu utatishiwa
Mkuu wa Baraza la Kistratijia la Mahusiano ya Kigeni la Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu italazimika kuangalia upya kanuni yake ya nyuklia iwapo utawala wa Kizayuni wa Israel utatishia uwepo na usalama wa taifa hili.
10 Mei 2024
Madai ya Marekani ya kusimamisha kuupelekea silaha utawala wa Kizayuni wa Israel
Waziri wa Ulinzi wa Marekani Lloyd Austin alidai siku ya Jumatano mbele ya Baraza la Seneti la nchi hiyo kwamba kuupelekea silaha utawala wa Kizayuni wa Israel kumesimamishwa kwa sababu ya utawala huo kutekeleza operesheni ya kuivamia kijeshi Rafah, lakini pamoja na hayo bado hawajachukua uamuzi rasmi kuhusu hatima ya shehena hiyo ya silaha.
10 Mei 2024
WHO: Mgogoro wa afya ya akili, ndilo janga 'lijalo' duniani
Afisa mwandamizi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) ametahadharisha kuwa, dunia ipo katika hatari ya kukumbwa na janga la matatizo ya afya ya akili.
10 Mei 2024
Njama za utawala wa Kizayuni za kuzusha mgogoro wa kibinadamu Rafah
Katika kuendeleza jinai zake utawala wa Kizayuni umepanga kuzusha mgogoro wa kibinadamu huko Rafah.
8 Mei 2024
Utafiti: Wahamiaji nchini Ujerumani wanakabiliwa na umaskini kutokana na ubaguzi wa rangi
Utafiti mpya umebaini kuwa, wahamiaji nchini Ujerumani wanakabiliwa na hatari kubwa ya umaskini kutokana na ubaguzi wa rangi. Haya ni kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Kituo cha Utangamano na Utafiti wa Masuala ya Wahamiaji cha Ujerumani.
8 Mei 2024
HRW yaikosoa Marekani kwa kuupa silaha utawala wa Kizayuni
Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch (HRW) limetangaza katika ripoti yake kuwa Israel imetumia silaha kutoka Marekani katika mashambulizi yake dhidi ya eneo la al Habariyeh huko Lebanon.
8 Mei 2024
Wataalamu wa hali ya Hewa: Mwezi Aprili dunia iliathiriwa na joto kali
Kitengo cha ufuatiliaji wa hali ya hewa cha Ulaya kimeeeleza kuwa dunia ilikumbwa na joto kali mwezi Aprili mwaka huu; kiwango ambacho kimetajwa kuwa ni muendelezo mtawalia wa hali ya joto kali kwa muda wa miezi 11 ambayo haijawahi kushuhudiwa.
8 Mei 2024
Bahamas yaitambua rasmi Palestina kama nchi
Wizara ya Mambo ya Nje ya Bahamas imetangaza rasmi kuwa inaitambua rasmi Palestina kama nchi.