Maadhimisho ya kuzaliwa kwa Imam Mahdi (a.t.f.s) yaliyoambatana na 15 Shaaban yalifanyika tarehe 04/02/2026 mjini Moshi, Tanzania, kwa kushirikisha waumini wengi. Khatibu, Samahat Sheikh Miraji Salim, alieleza kwa kina neema ya uwepo wa Imam Mahdi (a.t.f.s) kama Baqiyyatullah katika ardhi ya Mwenyezi Mungu, na akawahimiza waumini kujiandaa kiroho na kimaadili katika kumngojea kwa vitendo, si kwa maneno pekee.