Adabu
-
Usijivune kwa Maneno Maneno na Kujiona Mwenye Fadhila | Ibada na Jema lolote bila Unyenyekevu, ni Njia ya kupoteza kila Kheri
Baadhi ya Mabedui walikuwa wakimfanyia Mtume (s.a.w.a) madai ya fadhila kwa kusilimu kwao, kama Qur’ani inavyosema: “Wanakuonea fadhila kwa kusilimu kwao.” Basi Qur’ani ikawafunza adabu kwa kusema: “Sema: Msinionee fadhila kwa Uislamu wenu; bali Allah ndiye anayekuoneeni fadhila kwa kuwaongoza kwenye imani, ikiwa nyinyi ni wakweli.” (Al-Hujurāt: 17).
-
Jamii bora haihitajii watu ambao ni wasomi, bali inahitajia watu walioelimika | "Elimu bila Adabu ni sawa na Upanga Mkali Mikononi mwa Kichaa"
Msemo huu: "Elimika Usiwe Msomi" ni wito wa kuhusisha Elimu na Maadili. Elimu ya Kweli huonekana katika namna unavyowatendea wengine. Namna unavyofikiri kuhusu Haki na Uadilifu kwa kila Mwanadamu bila kujali Imani yake ya Kidini.
-
Siri na Falsafa ya Ratiba ya Darsa ya "Subhi ya Kimaanawi" kwa Wanafunzi wa Jamiat Al-Mustafa, Dar-es-Salam, Tanzania + Picha
Maulamaa wakubwa katika historia zao, walikuwa wakitafuta Adabu (Maadili) kwanza, kisha ndio wanaitafuta elimu. Wengine walikuwa wakiitafuta adabu kwa muda wa miaka 30, na elimu wanaitafuta kwa muda wa miaka 20.