Msemo huu: "Elimika Usiwe Msomi" ni wito wa kuhusisha Elimu na Maadili. Elimu ya Kweli huonekana katika namna unavyowatendea wengine. Namna unavyofikiri kuhusu Haki na Uadilifu kwa kila Mwanadamu bila kujali Imani yake ya Kidini.
Maulamaa wakubwa katika historia zao, walikuwa wakitafuta Adabu (Maadili) kwanza, kisha ndio wanaitafuta elimu. Wengine walikuwa wakiitafuta adabu kwa muda wa miaka 30, na elimu wanaitafuta kwa muda wa miaka 20.