Makao Makuu ya Khatam al-Anbiyaa (as) yamesema wananchi wa Iran na vikosi vyao vya ulinzi, kwa msaada wa Mwenyezi Mungu na chini ya uongozi wa Amiri Jeshi Mkuu, vimethibitisha kuwa Marekani na Israel hawana njia nyingine isipokuwa kukiri kushindwa na kusalimu amri mbele ya uthabiti wa taifa la Iran.
Katika hafla hii, washairi walitumia lugha ya fasaha na yenye kugusa hisia kueleza hadhi ya mashahidi, wakisoma mashairi yenye maudhui ya hisia, ujasiri na ucha Mungu, ambayo yalionyesha sio tu upendo wa kibinadamu bali pia dhamira ya kijamii, mwamko wa kiutamaduni na mshikamano wa kitaifa.