Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran (AEOI) limetangaza kuwa linakaribia kuzindua rasmi AlphaZa, dawa ya kwanza iliyotengenezwa nchini humo kwa kutumia teknolojia ya mionzi ya alpha, inayolenga kutibu saratani zilizo katika hatua za juu na zinazoshindikana kwa matibabu ya kawaida. Hatua hiyo inaashiria mafanikio makubwa ya Iran katika matumizi ya amani ya teknolojia ya nyuklia katika sekta ya afya.