Ilham Aliyev, Rais wa Azerbaijan, ametangaza kuwa nchi yake haina mpango wa kutuma vikosi vyake kushiriki katika operesheni za kulinda amani nje ya mipaka ya nchi, ikiwemo Gaza.
Uturuki imetangaza rasmi kuwa imefungia anga lake kwa ndege za Israel, ikiwa ni pamoja na ndege ya Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu, na haitatoa ruhusa yoyote kwa safari yake kwenda Azerbaijan. Hatua hii imechukuliwa kutokana na sera za utawala wa Israel kuhusu Gaza, na Uturuki inaendelea kuunga mkono haki za watu wa Palestina.