Shirika la Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) kupitia Tamko la Baku limesisitiza juu ya umuhimu wa kuimarisha sekta za ubunifu na diplomasia ya kitamaduni katika ulimwengu wa Kiislamu.
Uturuki imetangaza rasmi kuwa imefungia anga lake kwa ndege za Israel, ikiwa ni pamoja na ndege ya Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu, na haitatoa ruhusa yoyote kwa safari yake kwenda Azerbaijan. Hatua hii imechukuliwa kutokana na sera za utawala wa Israel kuhusu Gaza, na Uturuki inaendelea kuunga mkono haki za watu wa Palestina.