Akinukuu Aya ya 108 ya Surah Yusuf, Sheikh Ghawth alisisitiza umuhimu wa kutumia akili, mazingatio na dalili za ulimwengu wa nje (Ulimwengu wa Dhahiri) katika kumuelewa Muumba.
Watu wengi wanatamani Maisha ya Hawza na wanachukua uamuzi wa kujiunga katika Seminari/ Hawza ili kupata Elimu na Maarifa yenye uwezo mkubwa wa kumuongoza Mwanadamu na hatimaye kuchukua kikamilifu mtindo wa Maisha ya Hawza.