Majina haya ya heshima (Lakabu) hayakuwa tu kwa lengo la kuitana (ili mradi kuitana, pasina kuwepo kigezo chochote cha msingi), bali yalibeba taarifa za kiroho, madhumuni ya uongozi wa ki_Mungu, na mafunzo kwa Waislamu wote. Kujifunza kuhusu laqabu za Imamu Ridha (a.s) ni kujifunza kuhusu maisha na tabia bora za Kiislamu.
Hafla hii imehudhuriwa na Madrasat kutoka Bilal Muslim – Kanda ya Pangani pamoja na baadhi ya Madrasa kutoka kwa ndugu zetu wa Kisuni. Hili ni jambo la faraja kubwa, linaloashiria mshikamano wa kijamii na wa kidini katika maeneo yetu.
Wasomaji wa Kitaifa na Kimataifa wa Qur'an Tukufu wa Tanzania pamoja na Masheikh waliotoka maeneo mbalimbali ya nchi, ni miongoni mwa waliodhuhuria katika Hafla hiyo adhimu.