Italia
-
Marekani yaiondoa ndege yake ya upelelezi MQ-4C Triton kutoka Jordan kuelekea Italia baada ya mashambulizi ya Iran
Ripoti zinaeleza kuwa Marekani imeiondoa ndege yake ya kisasa ya upelelezi aina ya MQ-4C Triton kutoka Jordan na kuihamishia Italia, hatua inayokuja baada ya mashambulizi ya Iran dhidi ya vituo vya kijeshi vya Marekani katika eneo la Mashariki ya Kati.
-
Meloni Aishukuru Qatar na Pakistan kwa Kufanikisha Makubaliano ya Marekani na Iran
Waziri Mkuu wa Italia, Giorgia Meloni, ameishukuru Qatar, Pakistan na wapatanishi wengine kwa mchango wao katika kufanikisha makubaliano kati ya Marekani na Iran, akisema juhudi zao zimefungua ukurasa mpya wa diplomasia na amani katika eneo la Mashariki ya Kati.
-
Italia na Hispania Zimetuma Manowari za Kivita kwa ajili ya Kulinda Msafara wa Meli za Sumuud
Kufuatia mashambulizi ya ndege zisizo na rubani (droni) dhidi ya msafara wa kimataifa wa Sumuud (Jina la Msafara), ambao unalenga kupeleka misaada ya kibinadamu kwa Gaza na ulikuwa ukisafiri katika maji ya kimataifa, Italia na Uhispania zimetuma meli zao za kivita ili kuhakikisha usalama wa msafara huo. Hatua hii imechukuliwa baada ya kulaaniwa kwa kiwango kikubwa kwa mashambulizi hayo dhidi ya meli zisizo za kijeshi, ambayo yamechukuliwa kuwa ni uvunjaji wa sheria za kimataifa.
-
Jeshi la Italia Lakamata Meli ya Mizigo ya Silaha Inayodaiwa Kutoka Saudi Arabia Kwenda Israel
Kwa mujibu wa vyanzo vya usalama, silaha hizo zinadaiwa kuwa sehemu ya mpango mpana wa usafirishaji wa vifaa vya kijeshi kuelekea Israel, wakati huu ambapo mapigano na mashambulizi katika Ukanda wa Gaza yanaendelea.