Khoja

  • Jumuiya ya Waislamu wa Shis Khoja Ithna Ashari Jamiat katika Matembezi ya A'shura

    Jumuiya ya Waislamu wa Shis Khoja Ithna Ashari Jamiat katika Matembezi ya A'shura

    ASHURA ni siku ya kumi ya mwezi mtukufu wa Muharram. Katika siku hii ya Ashura mjukuu wa Mtume yaani Imam Hussain (as) aliuawa katika tambarare za mji wa Karbala baada ya kusimama kidete dhidi ya mtawala dhalimu wa wakati ule, Yazid bin Muawiya, akatoa fundisho la kukataa kumpigia magoti mdhalimu huyo, ndipo akajitolea maisha yake, akauawa ili kunusuru ubinaadamu , utu pamoja na kupigania uislamu.