Kibri cha dhalimu huyu (Marekani/Trump) hakimaanishi kwamba Mwenyezi Mungu amempuuza au amemsahau. Kinyume chake, kadiri dhalimu anavyozidi kujipandisha juu kwa kibri na majivuno, ndivyo anguko lake linavyozidi kuwa la kutisha zaidi.
Kibri ni ugonjwa wa moyo unaoharibu uhusiano wa mwanadamu na Allah, watu, na hata nafsi yake. Kwa mwanafunzi wa Hawza, kibri ni hatari zaidi kwani huua baraka ya elimu na huzuia nuru ya maarifa kuingia moyoni. Njia ya wokovu ni unyenyekevu (tawadhu’), kwani Mwenyezi Mungu huwanyanyua walio wanyenyekevu na kuwashusha wenye kibri.