Jeshi la Iran limetangaza kuwa katika hatua ya 13 ya Operesheni "Saa'iqah", vikosi vyake vya majini vilirusha kombora la cruise kuelekea meli ya kijeshi ya Marekani kaskazini mwa Bahari ya Hindi, likisema hatua hiyo ilisababisha meli hiyo kujiondoa kutoka eneo hilo.
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran (IRGC) limesema limelenga kambi ya kijeshi ya Marekani baada ya shambulizi lililoripotiwa kufanywa karibu na Uwanja wa Ndege wa Bandar Abbas, likionya kuwa uchokozi wowote dhidi ya Iran utakabiliwa na majibu makali zaidi.