Kwa mujibu wa wachambuzi, ushiriki wa mamilioni ya wananchi wa Iran katika maandamano na mikusanyiko ya kuunga mkono Jamhuri ya Kiislamu ni ishara ya mshikamano wa ndani na jibu la kisiasa kwa vitisho vinavyozidi kuongezeka kutoka Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel.
Kauli ya Donald Trump, rais wa Marekani, iliyokiri wazi kiwango cha msaada mkubwa wa Marekani kwa Israel, imezua mjadala mpana katika uwanja wa siasa za kimataifa. Wachambuzi wanasema kauli hiyo inaashiria ushiriki wa moja kwa moja wa Marekani katika sera na hatua zinazohusishwa na ukaliaji wa ardhi, uvamizi na ukiukwaji wa haki za binadamu dhidi ya wananchi wa Palestina, jambo lililoibua maswali mazito kuhusu uwajibikaji wa kimaadili na kisheria wa Washington mbele ya jumuiya ya kimataifa.