Walinzi wa Mapinduzi wakiionya Uingereza:
“Tunauonya utawala wa kifalme wa Uingereza, ambao umekuwa sababu kuu ya mateso ya watu wa eneo letu, una historia nyeusi ya kugawanya nchi za Kiislamu na kuhusika katika mauaji makubwa katika nchi hizo, pamoja na kushiriki kwa kiwango kikubwa katika mashambulizi ya hivi karibuni ya Marekani na utawala wa Kizayuni dhidi ya Iran, usifanye historia yake kuwa ya maangamizi na uovu mkubwa zaidi kuliko ilivyo.”