Madhalimu
-
Katika ujumbe kwa Mkutano wa Mwaka wa Umoja wa Vyama vya Wanafunzi wa Kiislamu barani Ulaya; Kiongozi wa Mapinduzi:
Hitaji kuu la dunia leo ni mfumo wa haki wa kitaifa na kimataifa wa Kiislamu / Shambulio la Marekani lilishindwa mbele ya ujasiri wa vijana wa Iran
Ayatollah Khamenei, katika ujumbe wake kwa Mkutano wa 59 wa Mwaka wa Umoja wa Vyama vya Wanafunzi wa Kiislamu barani Ulaya, amesisitiza kuwa sababu kuu ya msukosuko na wasiwasi wa madhalimu wafisadi si suala la nyuklia, bali ni kuinuliwa kwa bendera ya kupinga mfumo usio wa haki na utawala wa mabavu wa mfumo wa ubeberu duniani, pamoja na mwelekeo wa Iran ya Kiislamu kuelekea kujenga mfumo wa haki wa kitaifa na kimataifa wa Kiislamu.
-
Katika mkutano na kundi la wanafunzi wa vyuo vya kidini:
Sheikh Zakzaky atoa onyo kuhusu juhudi za kutengeneza “Uhusiano wa kawaida” ili kuhalalisha uhusiano na Madhalimu
Sheikh Zakzaky amesema: “Kama maridhiano na madhalimu yangekuwa sahihi, basi Imam Hussein (a.s) angekubaliana na Yazid.” Sheikh Ibrahim Zakzaky, katika mkutano na kundi la wanafunzi wa vyuo vya kidini kutoka nchi kadhaa za Kiislamu, alisisitiza wajibu wa kielimu na kijamii wa wanafunzi wa dini, akiwahimiza kujifunza kwa undani elimu za Kiislamu, kuielimisha jamii, na kulinda uhuru wa fikra. Aidha, alitoa onyo kali kuhusu juhudi za kuhalalisha au kuzoesha maridhiano na madhalimu.
-
Jinsi ya kuthibitisha Isma ya Maimamu 9 (a.s) kutoka ndani ya Qur’an Tukufu
“Na (Kumbukeni) Ibrahim alipojaribiwa na Mola wake kwa matamko, naye akayatimiza. Akasema: Hakika mimi nitakufanya kuwa Imam wa watu. Ibrahim akasema: Je,na Kizazi changu (pia)?.(Ndiyo, lakini) ahadi yangu haiwafikii Madhalimu.”