Katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, ambao ni karamu ya Mwenyezi Mungu, “brand” ya kweli si mavazi ya gharama bali ni taqwa, ikhlasi, subira na maadili mema. Hivi ndivyo vinavyomfanya mja awe mrembo mbele ya Mwenyezi Mungu na kufuzu katika meza ya rehema na maghfira.
Swala ya jamaa ni mkusanyiko wa kifahari zaidi, bora zaidi, safi zaidi, na wa kiroho zaidi duniani. Kwa sababu hiyo, ina fadhila na thawabu nyingi. Kwa kila hatua anayopiga mtu kuelekea swala ya jamaa, huandikiwa thawabu na wema. Na iwapo idadi ya waswaliji itazidi watu kumi, basi hakuna ajuaye kiwango cha thawabu isipokuwa Mwenyezi Mungu tu.