Kamati ya Maandalizi ya Maridhiano Day 2026 imetoa tuzo za heshima kwa viongozi wa Mkoa wa Mwanza pamoja na Jeshi la Polisi, kama ishara ya kutambua mchango wao katika kudumisha amani, mshikamano na utulivu wa kijamii. Tuzo hizo zilitolewa katika hatua inayolenga kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi za serikali, vyombo vya ulinzi na jamii kwa ujumla kuelekea maandalizi ya tukio hilo muhimu la Maridhiano Day 2026.