Mwakilishi wa Kiongozi Mkuu wa Kidini katika Masuala ya Hija na Ziara, katika hafla ya kufunga tukio la pili la kimataifa la vyombo vya habari “Nahnu Abna’ Al-Husayn (a.s)”, alisisitiza umuhimu wa kunufaika na mtindo wa maisha na mafundisho ya Imam Husayn (a.s) ili kujibu mahitaji ya jamii ya leo.
"Mashambulizi ya Kitamaduni hayako tena katika kiwango cha tahadhari au nadharia; leo hii yamejikita katika kona za fikra za kijana wa Kiiran na kwa utulivu, lakini kwa mfululizo, na yanashambulia imani, utambulisho na mtindo wa maisha ya Kiislamu."