Wakati Sweden ikiitaka Iran kufungua Mlango wa Hormuz kwa mujibu wa sheria za kimataifa, imekumbushwa shutuma za kusimamisha usafirishaji wa bandeji za Mepilex kwenda Iran chini ya vikwazo vya Marekani, hatua iliyodaiwa kuwaathiri vibaya watoto wanaougua maradhi ya EB maarufu kama “Butterfly Children.”
Katika ujumbe wake mzito kwa jumuiya ya kimataifa, Balozi Matinyi alisisitiza kuwa Tanzania ya sasa inatafuta wafanyabiashara na wawekezaji, si wafadhili. Taifa linaendelea kutekeleza miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo Reli ya Kisasa (SGR), pamoja na mradi wa gesi asilia unaokadiriwa kugharimu dola bilioni 42, miradi inayolenga kuimarisha uchumi wa taifa na nafasi yake katika uchumi wa kikanda na kimataifa.