Kwa mujibu wa wachambuzi, ushiriki wa mamilioni ya wananchi wa Iran katika maandamano na mikusanyiko ya kuunga mkono Jamhuri ya Kiislamu ni ishara ya mshikamano wa ndani na jibu la kisiasa kwa vitisho vinavyozidi kuongezeka kutoka Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel.
Kiongozi huyo wa kidini wa Shia Pakistan alisisitiza kuwa leo hii, rushwa, ukosefu wa sheria na usimamizi mbovu ndizo zimeenea kote katika eneo la Gilgit-Baltistan. “Wananchi wanajiona wapo peke yao, wamenyimwa haki na hawana pa kutegemea. Endapo hali hii itaendelea, ghadhabu ya wananchi inaweza kubadilika na kuwa dhoruba kubwa ambayo mzigo wake utabebwa na watawala pekee,”