Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa wale wanaotumia machafuko kama njia ya kutawala mataifa mengine huishia kuwa watumwa wa machafuko hayo. Ameonya kwamba nguvu iliyoundwa kwa ajili ya kuwatawala wengine hatimaye huweza kutoka katika udhibiti wa walioiunda.
Ayatullah Khamenei amesisitiza utayari wa mazungumzo na waandamanaji halali, huku akionya kuwa wachochezi wa fujo—aliowataja kuwa mamluki wa adui—hawastahili mazungumzo na wanapaswa kuzuiwa kwa sababu ya kueneza kauli mbiu dhidi ya Uislamu, Iran na Jamhuri ya Kiislamu.