Wilayat

  • Waumini Wahimizwa Kuzidisha Ibada na Matendo ya Kheri katika Sikukuu ya Ghadir

    Waumini Wahimizwa Kuzidisha Ibada na Matendo ya Kheri katika Sikukuu ya Ghadir

    Sikukuu ya Ghadir, ambayo ni miongoni mwa sikukuu kubwa zaidi kwa Waislamu wa Madhehebu ya Shia Ithna Ashari, ambapo huadhimisha ndani yake kutangazwa kwa wilayat ya Imam Ali ibn Abi Talib(as). Katika siku hii, Waumini huhimizwa kufanya amali mbalimbali za ibada na kheri kama vile kuswali, kusoma dua, kutoa sadaka na kuwalisha wengine, huku wakitumia fursa hiyo kuimarisha maarifa ya dini, kuhuisha ahadi yao katika kushikamana na Ahlul-Bayt (a.s) na kuimarisha mshikamano wa kijamii na kiroho.

  • Wilayat ya Amīr al-Mu’minīn (a.s) katika kauli za Imam Muhammad al-Baqir (as)

    Wilayat ya Amīr al-Mu’minīn (a.s) katika kauli za Imam Muhammad al-Baqir (as)

    Wilaya kwa maana ya upendo na utiifu: Wilaya ya Ali ibn Abi Talib ina maana ya upendo wa moyo na utiifu wa vitendo kwa kiongozi huyu katika nyanja zote za maisha. Wilaya kwa maana ya njia ya uongozi na mwongozo: Wilaya ya Ali ibn Abi Talib (as) ni mwakilishi wa kuendelea kwa njia ya Nabuwat / Unabii na mwongozo wa Kiungu baada ya Mtume (s.a.w.w), ikionyesha kwamba uongozi wake ni kielelezo cha mwongozo wa Mungu na mafundisho ya nabii.

  • Funzo Kuu la Arbaeen ni Msimamo Imara, Subira, na Mapambano: Ayatollah Ramazani

    Funzo Kuu la Arbaeen ni Msimamo Imara, Subira, na Mapambano: Ayatollah Ramazani

    Mkutano wa awali wa wavuti (webinar) ulioandaliwa na Idara ya Masuala ya Kimataifa ya Jumuiya ya Kimataifa ya AhlulBayt (a.s.) kuhusu mada “Kutathmini Ujumbe wa Kimataifa wa Arbaeen ya Imam Hussain (a.s): Kutoka Wilayat hadi Wajibu” umefanyika.