Ripoti zinaeleza kuwa Iran inaendelea kusimama kidete katika msimamo wake wa kutoruhusu akiba yake ya urani iliyorutubishwa kuhamishwa nje ya nchi, jambo linaloongeza ugumu katika mazungumzo yanayoendelea na Marekani kuhusu makubaliano mapya ya nyuklia na usalama wa kikanda.
Kwa mujibu wa ripoti ya Politico, Marekani inajizuia kuchukua hatua ya kijeshi dhidi ya Iran kutokana na hofu ya kupungua kwa akiba ya silaha na uwezekano wa wanajeshi wake kuuawa au kujeruhiwa, huku mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja yakiendelea mjini Geneva kwa upatanishi wa Oman.