awali
-
Mazungumzo yaendelea kwa ajili ya kufikia makubaliano ya kunyang’anya silaha Gaza / Kikosi cha Indonesia chatarajiwa kuwasili mwezi Machi
Katika muktadha wa kunyang’anya silaha huko Gaza, mapendekezo mengi yamewasilishwa. Inabakia kuonekana iwapo Hamas na makundi ya muqawama watakubali kikamilifu suala hili. Hapo awali, mazungumzo yalihusu tu silaha nzito, lakini sasa yanajumuisha pia silaha za mtu binafsi.
-
Siri iliyofichuliwa na wafungwa wa Palestina kutoka katika gereza la Israel kuhusiana na wafungwa waliopotea wa Lebanon
Baadhi ya waliokuwa huru wamesema kuwa walikutana na Walebanon waliokuwa wameorodheshwa awali kama waliopotea katika magereza ya Ofer, Nafha, Ramla, na Ashkelon.
-
Mwenyekiti wa Baraza la Wanazuoni wa Kishia wa Pakistan:
"Kuitambua tu Palestina hakutoshi - Hatua za vitendo pia ni muhimu"
Mwenyekiti wa Baraza la Wanazuoni wa Kishia wa Pakistan amesisitiza: "Nchi ambazo hapo awali zilikuwa kimya au hata ziliunga mkono utawala haramu wa Kizayuni (Israel), leo hii zinajifanya kupinga ukatili wa utawala huo na zinaanza kuutambua rasmi uhuru wa Palestina. Ingawa hii inaonekana kama hatua chanya kwa mtazamo wa nje, haitoshi kama haitafuatiwa na hatua madhubuti."